Jumamosi, 25 Aprili 2026

SOMO;MUNGU ANACHUKULIA NADHIRI KWA UZITO

​SOMO;MUNGU ANAICHUKULIA NADHIRI KWA UZITO SANA;


Nadhiri ni Kiapo cha Nafsi Ya Mtu na Mungu. Pasipo Kulazimishwa au Kushurutishwa Anaweza Kuweka Akiwa Peke yake Anakuja Kumpa Taarifa. 
Naitwa Pastor Richard Wa Morogoro

Madhara Makubwa Huwa Pale Usipotaka Kuitengua Nadhiri Yako. Jamani Nadhiri Usipoiondoa Huwa Mbaya Sana

Haya Maandiko Yanatuongoza Hebu Tuyasome Mwanangu. 

Mbaya ni Wale Watu Wanaosema Baba Niombee Nikipata Kazi Sitaacha Madhabahu Hii Kutoa Zaka Akishapata Kazi Hufanyii Kazi. 

Tuwe Makini Na Vinywa Vyetu Tusiwe Tunaweka Nadhiri Mgumu mfano unasema nikipata Kazi nitajitoa kwa wahitaji kila mwezi mshahara Wenyewe ukija kuugawa unashindwa kutembea na Nadhiri Hiyo

Acha Kukurupuka Kuweka Nadhiri


1. Umuhimu wa Kutimiza Nadhiri Kwa Wakati



  • Mhubiri 5:4-5: "Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; kwa kuwa yeye hana furaha na wapumbavu; iondoe hiyo uliyoinadhiri. Ni afadhali usiweke nadhiri, kuliko kuiweka usiondoe."

  • Zaburi 50:14: "Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; mtimizie Aliye Juu nadhiri zako."

  • Zaburi 66:13-14: "Nitaiingia nyumba yako na sadaka za kuteketezwa, nitakutimizia nadhiri zangu, ambazo midomo yangu ilizisema, na kinywa changu kilizinena, nilipokuwa katika shida."

​2. Nadhiri ni Hiari lakini ni Lazima Itimizwe



  • Kumbukumbu la Torati 23:21-23:

  • "Utakapoweka nadhiri kwa Bwana, Mungu wako, usiwe mlegevu katika kuiondoa; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, atauliza kwako hakika; nayo itakuwa dhambi kwako. Lakini ukijizuia usiweke nadhiri, haitakuwa dhambi kwako. Yaliyotoka midomoni mwako yashike na kuyatenda..."

​3. Tahadhari ya Kukurupuka


  • Mithali 20:25: "Ni mtego kwa mtu kusema kwa haraka, Kitu hiki ni kitakatifu, na baada ya kuweka nadhiri kuanza kuuliza-uliza."

​4. Mifano ya Nadhiri Katika Biblia


  • 1 Samweli 1:11 (Hana): 

  • "Akaweka nadhiri, akasema, Ee Bwana wa majeshi, ikiwa wewe utaliangalia teso la mjakazi wako... na kunipa mimi mjakazi wako mtoto mwanamume, ndipo mimi nitakapomtoa kwa Bwana siku zote za maisha yake..."

  • Mwanzo 28:20-22 (Yakobo): 

  • "Yakobo akaweka nadhiri akisema, Mungu akiwa pamoja nami... basi hili jiwe nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi."

HITIMISHO

Usiichukulie Kimzaha Nadhiri Sababu Inatesa Sana Utawapa Kazi Kuanza Wachungaji Kuvunja roho Kuvunja laana Kumbe Siyo Laana Ni Nadhiri Kunawengine Anapitia Matatizo Yaliyosababishwa Na Nadhiri. 

Jiseach Ndani Yako Ujiangalie Nadhiri Ambayo uliweka Uliendoa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni