SOMO:ZIFAHAMU GROUP (KUNDI) ZA DAMU PAMOJA NA AINA YA ULAJI NA TABIA ZAKE.
Vitabu: Mithali:3:8 Mithali;4:22
Yeremia 33:6
Tazama, nitauletea afya na kupona, nami nitawaponya; nami nitawafunulia wingi wa amani na kweli.
๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐
Kundi lako la damu linaweza kukufanya uwe dhaifu au imara katika kukabiliana na magonjwa fulani.Ni vema kujua kundi lako la damu sawa na ilivyo vema kujua mambo mengine yanayochangia kuwa na afya njema. Kujua kundi lako la damu Kunaweza kukuza uwezo wako wa kufahamu hatari zinazo kukabili kutokana na kundi la damu Ulilo nalo na kuepuka hatari hizo kwa kutumia mtindo wa maisha unaofaa.Hata hivyo, Kama vilivyo viungo vingine vya mwili, damu nayo ina changamoto ya kukumbana na maradhi mbalimbali, magonjwa yanayoathiri utendaji kazi wa damu yanaweza kugawanywa katika makundi kama vile ya kurithi, kuambukiza, mabadiliko ya kimwili na saratani tofauti.
Damu ya binadamu imegawanyika katika makundi makuu manne ambayo ni A, B, AB, na O, binadamu yeyote lazima awe na moja wapo ya makundi hayo.
Naitwa Pastor Richard Wa Morogoro
Kanisa la Holy Spirit Church Tanzania
GROUP- A (A+)
✔Hawa ni vegetarians. Yaani wala mboga mboga hasa za kijani. Pia wanahitaji sana mananasi na zabibu kwa wingi.
✔ Mara nyingi ni wale watu ambao hawaambiliki yaani wakiamua kitu wameamua mpaka wakitekeleze hata kama ni kibaya.
✔ pia ni watu ambao ni wabishi sana au wabishani na hawakubali kushindwa hivi hivi.
✔Watu Wa kundi hili pia huwa wana changamoto ya kuwa na upungufu Wa acid mwilini hivyo hushindwa kuiprocess protini tumboni hasa itokanayo na nyama nyekundu.
✔Ni watu ambao hushambuliwa sana na saratani za mishipa ya fahamu,utumbo,mifuko ya mayai,mfuko wa kizazi na mlango wa uzazi kwa wanawake,kibofu cha mkojo,figo,kongosho na saratani ya kinywa, tezi za mate na umio.
✔Wana hatari pia ya kupatwa na magonjwa ya Moyo,kupata lehemu mbaya mwilini,kwenye Moyo,wako hatarini pia kupata kiharusi na ugonjwa Wa shinikizo la damu Wa Moyo.
✔️Vyakula wanavyotakiwa kula kwa wingi ni mbogamboga za Majani na nyama nyeupe nyama nyekundu sio nzuri sana kwa watu hawa.
☑ ✔️Hawatakiwi kugusa kabisa au kutumia Mara kwa Mara vyakula hivi :-nyama nyekundu,ngano,machungwa,na maziwa
✔️ wakila ndizi,maembe na mapapai huwasababishia waamkapo asubuhi kutokwa na makamasi kwa wingi.
✔️Watu wa kundi hili wanapenda sana wali na Mara nyingi ndio Chakula chao kikuu.
Hawatakiwi kugusa kabisa ngano na mahindi na endapo wakatumia vyakula hivi hasa kwa wanawake huwasababishia kupata hedhi Mara mbili kwa mwezi.
Tabia zao ni hizi hapa:-
๐ni watu Wa gharama sana hasa wadada au wanawake.
๐huishiwa au wanakuwa na upungufu Wa damu sana..
๐ni wavivu nikiwa na maana hawawezi Kazi ngumu ngumu.
๐Ni waongo sana na sio wadanganyifu,ni wakweli (they don't like cheating)
๐ni wasiri sana.
๐wanapenda kujifichajificha kama ni usiku hupenda kukaa gizani sana.
๐ni waaminifu sana na hapa Mara nyingi unawakuta Maafisa utumishi kwani hufuata sheria.
๐Ni watu ambao pia wanaumwa Mara kwa Mara, kutokana na upungufu wa mwilini.
๐Wanapenda kuwa wao wao.Ni watu ambao wanafanya maamuzi wakiwa pekeyao.
๐Sio wazurulaji(Anaweza jifungia ndani asubuh mpaka jioni na ukadhani hamna mtu)
. ๐Wakipenda wanapenda kweli.
๐Wanahitaji handle with care, tunapokuja kuongelea mahusiano. Wanadeka mnoo.
GROUP _B (B+)
✔Hili ni kundi la watu ambao ni wazungumzaji yaani ukiwapa nafasi ya kuzungumza ni kama vile umekosea na hapa Mara nyingi unawapata watu kama MCs, Wasanii, Radio presenters.
✔Ni watu ambao wana tabia zilizojitosheleza yaan wamekamilika.
✔ Wanapenda kuonekana ,hapa utawakuta waimbaji Na watangazaji.
✔Ni watu ambao husumbuliwa sana au wako hatarini kupata magonjwa kama uvimbe Wa fizi,na pia wanawake walioko katika kundi hili wako hatarini kupata ugonjwa Wa kisukari aina ya pili.
✔ Mara nyingi ni watu ambao wakipata maambukizi ya virusi vya aina yoyote ile huwa machizi au vichaa kutokana na kwamba vinaenda kuharibu mfumo wake Wa fahamu, wana uwezo mkubwa kukabiliana na ugonjwa wa kipindupindu.
✔Wana hatari kubwa ya kupata saratani ya koo.
✔️Watu Wa kundi hili hawashauriwi sana kula vyakula vya aina ya kuku(Mara nyingi wao wenyewe tu hawapendi kuku ingawa hawaruhusiwi kula),Karanga,korosho,na nyanya, hizi pia hawashautiwi kula.
✔Ni watu ambao wanaamini sana kupitia maamuzi yao binafsi.
✔Si rahisi kuingia katika project yeyote unless, umempa derails za kutosha kuhusiana na hiyo project.
✔Ni watu wa malengo, yuko radio kupambana kuhakikisha anapata matokeo.
GROUP- AB(AB+)
✔Hawa ni watu ambao Mara nyingi hawaeleweki yaani wana tabia za A na pia tabia za B wakati mwingine.
✔Kundi hili la Damu husadikika ni kundi linalopenda sana dini. Na mara nyingi washehe, mapadre, wachungaji utakuta wengi wapo kundi hili.
✔Ni wakarimu sana na wanapenda sana watu.
✔Hujitolea kwa ajili ya wengine. Mtu wa jamii hii anaweza kukupa kila kitu akabaki hana yeye.
✔Ni watu ambao wanaweza akaanzisha kitu asikimalizie ukakuta kaishia katikati halafu kaanzisha kingine.
✔Ni watu ambao wako hatarini Kupata magonjwa kama kiharusi,dengue,magonjwa ya Moyo,shinikizo la Moyo,na lehemu kujaa kwenye mishipa ya damu.
✔Watu Wa kundi hili Mara nyingi wakifikia uzeeni uwezo wao Wa kufikiri hupungua kwa haraka.Lakini Mara nyingi kupungua kwa uwezo Wa kufikiri hutokana na magonjwa kama shinikizo la Moyo,kisukari na lehemu kuwa nyingi sana mwilini.
✔ ni watu ambao wana uwezo mkubwa sana Wa kukabiliana na magonjwa yaani kinga yao ya mwili ni imara ukifananisha na makundi mengine yote ya damu.
✔Ni watu ambao wako na hasira za ndani kwa ndani sio rahisi kuexpose hasira zake ukamtambua kirahisi.
✔Hubadilika kulingana na mazngira(Hawana tofauti na vinyonga).
✔Wanasifa ya uongozi.
GROUP -O(0+)
✔Hawa ni watu ambao ni jeuri na kiburi na wanajiamini sana.
✔Wanasifa ya uongozi. Wanapenda kuongoza watu(They're Leaders).
✔Wazurulaji mono.
✔Wako very much Open minded. Yaani ni watu wa Kureason mambo.
✔Watu ambao ni wababe,wagumu, na wanafanya maamuzi yao pale wanapoamua na sio kulazimishwa.
✔watu ambao wana roho nzuri sana ila hawapendi uongo hivyo usije ukajaribu kuwadanganya hata siku moja.
✔Ni watu ambao wanaweza jihusisha na mahusiano zaidi ya moja na wakaona wako sawa.
✔Ni Watu ambao sio rahisi sana kupata shambulio la ghafla la Moyo kama ilivyo kwa watu wenye makundi mengine ya damu.
✔Hawana kinga ya kutosha dhidi ya kipindupindu lakini wana kiasi fulani cha kinga dhidi ya Kifua Kikuu (TB), Malaria isiyo kali, saratani za kongosho, tumbo, matiti na mlango wa kizazi.
✔Ni rahisi kupata magonjwa ya maambukizi ya ngozi,na vidonda vya tumbo.Wanapata sana maumivu ya kiuno,magoti pamoja na mgongo.
✔Ni watu wasiopenda vitu vichachu kutokana na uwepo Wa acid kwa wingi mwilini mwao hivyo wanasumbuliwa sana na vidonda vya tumbo na huwa wanasumbuliwa sana na tatizo la choo (constipation) pamoja na kisukari.
✔Kundi hili pia hutokewa na mvi za mapema sana.
.
✔Kwa wanaume hapa ndipo unawakuta ambao wana mapaja yasiyolingana yaani moja kubwa lingine Dogo.
✔️Hawatakiwi kula ngano na mahindi Mara kwa Mara au kutokula kabisa.
✔️Hawapaswi kabisa kugusa au kula machungwa,passions,ukwaju,maembe mabichi, zabibu nk na vyote vyenye acid.
✔️Hawatakiwi kabisa kula ugali au wali,mahindi ya kuchoma au kukaanga au kupika hayawafai kabisa.
✔️Wanaume walioko katika kundi hili wanahitaji protein kwa wingi kuliko wanawake kutokana na kuhitaji nguvu kwa sana katika shughuli zao na miili yao kwa ujumla.
✔️Kwa wanaume wanatakiwa kula matunda sana kama maembe,mananasi,ndizi,matikiti maji (ule na mbegu zake) hapa pia kama ni tunda unakula lote mfano nanasi unalimaliza,papai unalimaliza,na pia matunda ya rangi moja kula kwa pamoja.
✔️Ukitengeneza kitu kama juice ya matunda unywe yote kwa wakati huo na sio kutengeneza ya wiki au siku kadhaa.
✔️Vyakula vinavyowasaidia au wanavyohitaji sana mwilini ni matunda ,mboga za Majani,protein kwa wingi yaani nyama,maharage,mayai na maziwa.
" HITIMISHO"
::::::::::::::::;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;:::::;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;
Magonjwa mengi yanaweza kuepukwa kwa kuzingatia usafi wa mwili na mazingira, mlo kamili(kula kilingana na Uhitaji wa group lako la damu), kufanya mazoezi, kupunguza uzito uliozidi na kuepuka matumizi ya tumbaku, pombe pamoja na madawa..*
Naitwa Pastor Richard wa Morogoro
Kanisa la Holy Spirit Church Tanzania
Morogoro Veta Dakawa