SOMO:MADHARA YA KUPITILIZA KUTEGUA NADHIRI.
1. Unatenda Dhambi
Biblia iko wazi kuwa kuchelewa kutimiza ulichoahidi ni dhambi.
"Utakapoweka nadhiri kwa Bwana, Mungu wako, usiwe mlegevu katika kuiondoa; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, hataacha kuitaka kwako; nayo itakuwa ni dhambi kwako." (Kumbukumbu la Torati 23:21)
2. Inaharibu Kazi ya Mikono Yako
Mungu hapendezwi na mtu anayeahidi kisha anaghairi au anachelewa bila sababu yako binafsi. Hupelekea Mambo yako kuharibika
"Usikiache kinywa chako kikukoseshe mwili wako; wala usiseme mbele ya mjumbe wa Mungu ya kuwa ni kosa; kwani Mungu akasirishwe na sauti yako, na kuiharibu kazi ya mikono yako?" (Mhubiri 5:6)
3. Kupoteza Sifa ya Kuwa Mwaminifu (Mtego wa Kiroho)
Kuchelewa kutimiza nadhiri kunamfanya mtu aonekane kama "mpumbavu" machoni pa Mungu kwa sababu ametoa ahadi ambayo hana nia ya kuitimiza haraka. Biblia inashauri ni afadhali usiahidi kuliko kuahidi na usilipe.
Hii Machoni Pake atajiona Mungu Atamsamehe number huwa hatia
"Ni heri usitoe nadhiri, kuliko kuitoa usiiitekeleze." (Mhubiri 5:5)
JE, UMEPUUZA NADHIRI AU UNAICHUKULIA RAHISI RAHISI NI BORA USIWEKE KULIKO UWEKE UJE UCHELEWE
KESI NYINGI ZA WATU WANATESWA NA NADHIRI.
. OMBA TOBA KAMA UMEPITILIZA KUIFUTA NADHIRI.
Naitwa Pastor Richard
WhatsApp+255710889892
Holy Spirit Church Tanzania
Morogoro Veta Dakawa
Karibuni Tujue Namna Ya Kuomba Toba Kama Tulizembea Kutengua Nadhiri
Sala ya Toba kwa ajili ya Nadhiri
OMBA HIVI"Mungu Mwenyezi, Baba wa Rehema, nakuja mbele zako kwa unyenyekevu nikitambua ukuu wako na uaminifu wako usio na mwisho.
Ninakiri mbele zako leo kuwa niliweka nadhiri [taja hapa nadhiri uliyoweka kama unakumbuka], lakini nimechelewa kuitekeleza kama nilivyoahidi. Ninatubu kwa uzembe, kusahau, au kukosa uaminifu katika maneno ya kinywa changu.
Neno lako linasema ni heri nisiahidi kuliko kuahidi na nisilipe. Naomba unisamehe kwa kosa hili na usiruhusu kazi ya mikono yangu iharibike kwa sababu ya hatia hii. Damu ya Yesu Kristo initakase na kuniondolea mtego huu wa kiroho uliokuwa unanikabili.
Ee Bwana, nipe neema na njia ya kutimiza kile nilichokusudia, na ikiwa uwezo wangu umepungua, nakuomba unipe hekima ya kuikomboa nadhiri hii kwa namna inayokupendeza. Tangu sasa, ninaomba unipe moyo wa tahadhari nitakapokuja mbele zako na dhabihu ya midomo yangu.
Asante kwa kunisikia na kunisamehe, kwa maana wewe ni Mungu wa nafasi ya pili. Amina."
Jambo la Kuzingatia:
Baada ya kuomba sala hii, unapaswa kujisikia mwenye amani. Hatua inayofuata ni kufanya juhudi za dhati kuitimiza ile nadhiri haraka uwezavyo. Biblia inasisitiza kuwa toba ya kweli huambatana na matendo ya kurejesha pale tulipokosea.
Tengua Haraka Usiendelee Kupuuza au kuzembea Kutengua Nadhiri
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni