1:Yesu alipoletwa Hekaluni akiwa mtoto mchanga, ni nani aliyemtambua kuwa ndiye Masihi?
Jibu: Simeoni ( Luka 2:22-38 ).
SWALI:2
2. Ni mgombea gani ambaye hakuchaguliwa kwa wadhifa wa mtume baada ya Yuda Iskariote kujiua, kulingana na Matendo ya Mitume?
Jibu: Yusufu Barsaba (Matendo 1:24–25).
SWALI:3
3. Ni vikapu vingapi vilivyobaki baada ya Yesu kuwalisha wale 5,000?
Jibu: Vikapu 12 (Marko 8:19).
SWALI:4
4. Katika mfano unaopatikana katika Injili tatu kati ya nne, Yesu alilinganisha mbegu ya haradali na nini?
Jibu: Ufalme wa Mungu ( Mt. 21:43 ).
SWALI:5
5: Musa alikuwa na umri gani alipokufa, kulingana na kitabu cha Kumbukumbu la Torati?
Jibu: Miaka 120 (Kumbukumbu la Torati 34:5-7).
SWALI:6
6: Ni kijiji gani kilikuwa mahali pa kupaa kwa Yesu, kulingana na Luka?
Jibu: Bethania ( Marko 16:19).
SWALI:7
7. Ni nani anayefasiri maono ya Danieli ya kondoo mume na beberu katika Kitabu cha Danieli?
Jibu: Malaika Mkuu Gabrieli ( Danieli 8:5-7 ).
Jibu: Malkia Yezebeli (1 Wafalme: 31).
Nifanye nini ili niokolewe?
Unapaswa kuamini kwamba Yesu alidhabihu uhai wake kwa ajili ya dhambi zetu. (Matendo 16:30, 31; 1 Yohana 2:2) Hilo linamaanisha kuamini kwamba Yesu alikuwa mtu halisi na kwamba mambo yote ambayo simulizi la Biblia linasema kumhusu ni sahihi.
Jifunze kile ambacho Biblia inafundisha hasa. (2 Timotheo 3:15) Biblia inasema kwamba mtume Paulo na Sila walimwambia hivi mlinzi wa jela: “Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokolewa, wewe na watu wa nyumba yako.” Kisha, baada ya hapo, walianza kumfundisha mlinzi huyo wa jela “neno la Yehova.” a (Matendo 16:31, 32) Hilo linaonyesha kwamba mlinzi huyo wa jela hangeweza kumwamini Yesu bila kuwa na ujuzi wa msingi wa Neno la Mungu. Alihitaji kuwa na ujuzi sahihi wa Maandiko.—1 Timotheo 2:3, 4.
Tubu. (Matendo 3:19) Pia, lazima utubu, au uhuzunishwe sana, kuhusu mwenendo na mtazamo mbaya uliokuwa nao. Wengine wataona toba yako kadiri unavyoacha mazoea yanayomchukiza Mungu na unapofanya “matendo yanayoonyesha toba.”—Matendo 26:20.
Ubatizo. (Mathayo 28:19) Yesu alisema kwamba wale ambao watakuwa wanafunzi wake wanapaswa kubatizwa. Mlinzi wa jela aliyetajwa hapo awali alibatizwa. (Matendo 16:33) Vivyo hivyo, baada ya mtume Petro kufundisha umati mkubwa ukweli kumhusu Yesu, “wale waliokubali neno lake kwa furaha wakabatizwa.”—Matendo 2:40, 41.
Tii maagizo ya Yesu. (Waebrania 5:9) Wale ambao ‘wanashika mambo yote’ ambayo Yesu aliamuru wanaonyesha kupitia maisha yao kwamba wao ni wafuasi wake. (Mathayo 28:20) Wanakuwa “watendaji wa neno, na si wasikiaji tu.”—Yakobo 1:22.
Vumilia mpaka mwisho. (Marko 13:13) Wanafunzi wa Yesu ‘wanahitaji uvumilivu’ ili

Wanawake Katika Biblia—Tunaweza Kujifunza Nini Kutoka Kwao?
Jibu la Biblia
Katika Biblia, tunasoma kuhusu wanawake wengi ambao maisha yao yanatufundisha masomo yenye thamani. (Waroma 15:4; 2 Timotheo 3:16, 17) Makala hii inazungumzia kwa ufupi tu baadhi ya wanawake wanaotajwa katika Biblia. Wengi wao ni mifano mizuri ya kuiga. Wengine ni mifano ya kuonya.—1 Wakorintho 10:11; Waebrania 6:12.
Abigaili
Abigaili alikuwa nani? Alikuwa mke wa mwanamume mkatili aliyeitwa Nabali. Hata hivyo, Abigaili alikuwa mwenye busara na mnyenyekevu, na pia alikuwa mrembo kimwili na kiroho.—1 Samweli 25:3.
Alifanya nini? Abigaili alitenda kwa hekima na busara ili kuzuia msiba. Yeye na Nabali waliishi katika eneo ambalo Daudi, mfalme mtarajiwa wa Israeli, alikuwa akijificha. Daudi na wanaume wake walipokuwa huko, walilinda makundi ya kondoo ya Nabali yasiibiwe. Lakini Daudi alipowatuma wajumbe kumwomba Nabali chakula, Nabali aliwatukana na kukataa. Daudi alikasirika sana. Kwa hiyo, yeye na wanaume wake wakapanga kwenda kumuua Nabali na wanaume wote wa nyumba yake.—1 Samweli 25:10-12, 22.
Abigaili alitenda upesi aliposikia kile ambacho mume wake alikuwa amefanya. Aliwapa watumishi wake chakula wampelekee Daudi na wanaume wake, naye pia akawafuata ili kumwomba Daudi awaonyeshe rehema. (1 Samweli 25:14-19, 24-31) Daudi alipoona zawadi yake, unyenyekevu wake, na aliposikia ushauri wake wenye hekima, alitambua kwamba Mungu alimtumia ili kumzuia asimuue Nabali na wanaume wake. (1 Samweli 25:32, 33) Muda mfupi baada ya hapo, Nabali alikufa, naye Abigaili akawa mke wa Daudi.—1 Samweli 25:37-41.
Tunajifunza nini kutoka kwa Abigaili? Ingawa alikuwa mrembo na tajiri, Abigaili alikuwa na maoni yenye usawaziko kujihusu. Ili kudumisha amani, alikuwa tayari kuomba msamaha kwa jambo ambalo halikuwa kosa lake. Alishughulikia hali yenye kutisha kwa utulivu, busara, ujasiri, na alitumia nguvu zake za kufikiri.
▸Ili kupata habari zaidi kumhusu Abigaili, ona makala yenye kichwa, “Alitenda kwa Busara.”
1:Inakuwaje Tunapokufa?
Jibu la Biblia
2:SWALI: Huyu Yeshuruni ni nani kwenye biblia?. Na kwanini alinenepa na kumdharau mwamba wa wokovu wake (Kumb.32:15)?.
JIBU: Yeshuruni ni jina lingine la Taifa la Israeli lililotumika katika biblia ya kiyahudi hususani katika mashahiri,..Neno hili linaonekana mara 4 katika biblia soma (Kumbukumbu 32:15, 33:26, 33:5 na Isaya 44:2).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni