Alhamisi, 13 Juni 2024

SEMINA YA NDOA

SEMINA ZA NDOA


                                  SEMINA ZA NDOA
            JE NI  NINI HATIMA  YA  NDOA   YAKO?

Utangulizi: PANGA KUMALIZA  VIZURI
Andiko:         Mhubiri  7:7-8
Heri  Mwisho wa neno   kuliko mwanzo wake.
Ndoa   chanzo chake  ni Rohoni.Muasisi  wake ni mungu .Yoh.4:24 Mungu  ni Roho

Tunaishi katika  ndoa  (a)Kwa  Hekima    Mith.14:1
                                     (b)Kwa  Akili        1Pet 3:7
                                     (c)Kwa    Kutii      Efe .5:22-24
                                     (d)Kwa Upendo    Efe .5:25 -29
                                     (e)Kwa  kuheshimiana  Ebr.13:4;1Pet. 3:7b;Efe.5:33b  Staha.

Tena tukumbuke –Mpango halisi  wa mungu kuhusu wanandoa ni  huu:-
            (i) Mke  awe  msaada kwa  mumewe.        Mwa 2 ;18
            (ii)Mume amfurahie mke wa ujana siku zote.Ndoa iwe ni mahali pa furaha  Mhu.9:9  
(iiiMapendo  yawe  ni ya siku zote.Kusiwepo na  kuchukizana –chuki Mith 5:18-19

Ndoa  zetu  tujitaidi ziwe  na
(i)Sifa  njema      Mhu .7:1;2  Kor.6:3-4;Tujipatie sifa njema
(ii)Ndoa    zetu ziwe  mfano mzuri /kielelezo chema kwa
(a)Watoto wetu
(b)Waaminio
(c)Wayahudi  1kor 10;32 1tim .4:12.katika usemi,mwenendo ,imani ,upendo,na usafi .
(d) Wayunani
(e)Maisha  yatu  ya  ndoa kumpa mungu utukufu.1kor.10:31

Tunaweza  kuiga mfano mzuri  wa ndoa  za wazee wetu  kama  adamu, Ibrahimu, Isaka, Nuhu, Ayubu n.k. Ebr.13:7. Walimaliza  vizuri tunaona jamopa na magumu mengi, lakini walikuwa na mwisho mzuri.  Tuiige imani yao.
02. NDOA INA VITATU VYA AWALI.  Ambavyo kila mwanandoa     akivishinda__aandelea mbele kwa ushindi na ndoa hiyo inakua na kumaliza vyema.

KITUTA CHA KWANZA

Kumfahamu mwenzi wako wa ndoa.

Katika KITUTA hiki kunapatikana darasa la kuchukuliana na kuelekezana.

Jambo kubwa katika darasa hili ni wanandoa wote kuwa:-

(a)   Wa kweli kila mtu kwa mwenziwe.


(b)  Wa wazi bila kufichana kitu.

(c)   Wanyenyekevu kila mmoja kwa mwenzake.

Kwenye Eneo hili, mke atumie HEKIMA yake aliyopewa na Mungu Mith. 14:1 na BUSARA Mith. 19 :14.

Kusiwepo na kukosoana wala kudharauliana ama kulaumiana bali uvumilivu na kuelimisha kuwe na nafasi ya kwanza haswa katika HAKI  za mtu katika TENDO la NDOA.  IKor.7:2-5,

Mara nyingi wanaondoa  wachanga  si wastadi   wa TENDO la NDOA maana hawana ujuzi wala uzoefu ; wala hawajui kujizuia au kungojana ili wapate kufikia shibe  ya raha  yao kwa pamoja .


Vile vile hawajui hata namna (style)mbalimbali  za tendo la ndoa ambazo ziko kama 9na 4 maalum ambapo mke ni mjamzito (mgo –solo –mago –ina –wima –kichu –juu –mapa –kuge ,kistu )INAHITAJI  MOYO  WA   UNYENYEKEVU :ili wanandoa hawa wapate kujifnza  na kupata  uzoefu (experience) .Inahitaji  kocha  nao watajipa  uzoefu wao kwa kungojana  na kuchukuliana hadi  waufikie  ujuzi  wa TENDO  la NDOA katika  hali ya kutoshelezana.


Inawezekana mtu kufanya  tendo la  ndoa kwa dakika 5,au 10 au 20au 30 kwa ustadi akamtosheleza mwenzake – lakini inatofautiana mtu na mtu – pia inatofautiana katika maumbile, kwa mfano:-

-       Wanawake wanene wana namna yao na kiwango chao mpaka wafikie kutosheka

-       Wanawake wembamba nao wana namna yao hadi kufikia kilele

-       Na wale wa umbo la kati wana jinsi yao ili kufikia kilele



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni