Jumatatu, 30 Desemba 2024

KUMBUKUMBU YA MALIPO YA UWAJA KWA MAZENGO

TAR.30/12/2024

Umetuma TSh 200,000 na pesa ya kutolea TSh 6,121 kwenda 255710173054 - TAITASI CLEMENCE. Jumla ya Makato TSh 1,200. (Ada TSh 1,200, Tozo TSh 0), VAT TSh 183. Kumbukumbu no: 900361692050. 30/12/24 19:22. Salio lako jipya ni TSh 1,974. Asante kwa kutumia Mixx by Yas.


TAR.14/1/2025

Umetuma TSh 107,000 kwenda kwa 255710173054 - TAITASI CLEMENCE. Jumla ya Makato TSh 1,000. (Ada TSh 1,000, Tozo TSh 0), VAT TSh 153. Kumbukumbu no.: 901567871375. 14/01/25 20:57. Salio lako jipya ni TSh 2,986. Tumia Mixx by Yas Super App iliyoboreshwa. Kupakua: Android: goo.gl/hizdo


Tar.1/2/2025

Umetuma TSh 90,000 kwenda kwa 255710173054 - TAITASI CLEMENCE. Jumla ya Makato TSh 720. (Ada TSh 720, Tozo TSh 0), VAT TSh 110. Kumbukumbu no.: 481777836454. 31/01/25 18:08. Salio lako jipya ni TSh 1,067. Tumia Mixx by Yas Super App iliyoboreshwa. Kupakua: Android: goo.gl/hizdoh au IOS: apple.co/2xP7XSS





TAR.12/2/2025

CBC1GP0Y0OR Confirmed. TAITASI CLEMENCE has received Tsh 105000 on 12-FEB-25 16:50:04.257.

Nilimlipa sh.105000/=


IMEBAKI SH.160000

Jumamosi, 28 Desemba 2024

Ijue biblia


IJUE BIBLIA - Sehemu ya I






UTANGULIZI


Biblia ni nini?


Biblia ni mkusanyiko wa vitabu 66 vilivyo andikwa na waandishi tofauti-tofauti 40 kwa takribani miaka 1500. Waandishi walikuwa wafalme, wavuvi, makuhani, viongozi wa serikali, wakulima, wachungaji, na madaktari. Biblia ni kitabu cha ajabu! Pamoja na kwamba vitabu vyake vimeandikwa na waandishi wengi tena kwa muda mrefu sana, bado kuna mtiririko na muunganiko wa ajabu kuanzia kitabu cha kwanza hadi cha mwisho. Hivyo basi kwa ujumla wake Biblia imeandikwa na wanadamu chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu wa Mungu

“Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinenayaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.” (2 Petro 1: 20, 21)


MGAWANYIKO WA BIBLIA


Utangulizi


Biblia imegawanyika katika sehemu kuu mbili. Sehemu ya kwanza inaitwa agano la kale lenye jumla ya vitabu 39 na sehemu ya pili inaitwa agano jipya lenye jumla ya vitabu 27. Kisha ikagawanyika katika sehemu nane; nne za agano la kale na nne za agano jipya. Yesu Kristo ndiye mzungumzwaji mkuu katika biblia nzima. Huonekana kama Mwokozi, tumaini la kweli kwa wanadamu wote. Yeye mwenyewe (Yesu Kristo) alishuhudia kuwa ndiye mhusika (mzungumzwaji)  mkuu katika agano jipya

  1. Katika Mathayo 5: 17, 18 alisema, “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka, hata yote yatimie.” 
  2. Alipokuwa akitembea na wanafunzi wake kuelekea Emau baada ya kufufuka, Luka 24: 13-31 inasema “ ... Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii! Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake? Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe... 
  3. Kisha baadaye jioni alipokuwa akizungumza na wanafunzi wake aliwaambia “... hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi. Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko. Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.” 
  4. Katika Yohana 5:39 na 40, wakati Yesu anazungumza na Wayahudi alisema “Mwayachunguza maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndaniyake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima”

Zaidi sana, katika Ufunuo 19:10 biblia inasema “... kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii” Kwa maneno mengine, asili na kusudi halisi la unabii na maandiko yote ni kumtangaza au kumdhihirisha Yesu Kristo. Anguko na uhitaji wa wokovu kwa mwanadamu, hasa ndivyo vinavyo changia Kisto Yesu kudhihirishwa and kutangazwa kwenye maandiko ya Agano la Kale na Agano Jipya. Kupitia Yesu Kristo tunapata uzima wa milele (Yohana 10:10)

Agano la Kale


Agano la kale lina jumla ya vitabu 39 ambavyo vimegawanyika katika makundi makuu manne kama ifuatavyo:


NO.
MGAWANYIKO WA AGANO LA KALE (A.K)
NO.
VITABU HUSIKA NDANI YA MGAWANYIKO WA A.K
1.       
Vitabu vya Sheria
1.       
Mwanzo
2.       
Kutoka
3.       
Mambo ya Walawi
4.       
Hesabu
5.       
Kumbukumbu la Torati




2.       
Vitabu vya Kihistoria
1.       
Joshua
2.       
Waamuzi
3.       
Ruthu
4.       
1 Samweli
5.       
2 Samweli
6.       
1 Wafalme
7.       
2 Wafalme
8.       
1 Mambo ya Nyakati
9.       
2 Mambo ya Nyakati
10.   
Ezra
11.   
Nehemia
12.   
Esta




3.       
Vitabu vya Kiushairi
1.       
Ayubu
2.       
Zaburi
3.       
Mithali
4.       
Muhubiri




4.       
Vitabu vya Manabii


a)      Vitabu vya Manabii Wakubwa
1.       
Isaya
2.       
Yeremia
3.       
Ezekiel
4.       
Danieli


b)      Vitabu vya Manabii Wadogo
1.       
Hosea
2.       
Yoeli
3.       
Amosi
4.       
Obadia
5.       
Yona
6.       
Mika
7.       
Nahumu
8.       
Habakuki
9.       
Zefania
10.   
Hagai
11.   
Zekaria
12.   
Malaki







Agano la Jipya


Agano jipya lina jumla ya vitabu 27 ambavyo vimegawanyika katika makundi makuu manne kama ifuatavyo:


NO.
MGAWANYIKO WA AGANO LA JIPYA (A.J)
NO.
VITABU HUSIKA NDANI YA MGAWANYIKO WA A.J
1.       
Vitabu vya Kihistoria
1.       
Mathayo
2.       
Marko
3.       
Luka
4.       
Yohana
5.       
Matendo Ya Mitume




2.       
Nyaraka za Mtume Paulo
1.       
Warumi
2.       
1 Wakorintho
3.       
2 Wakorintho
4.       
Wagalatia
5.       
Waefeso
6.       
Wafilipi
7.       
Wakolosai
8.       
1 Wathesalonike
9.       
2 Wathesalonike
10.   
1 Timotheo
11.   
2 Timotheo
12.   
Tito
13.   
Filemoni




3.       
Nyaraka za Jumla (kwa watu wote)
1.       
Waebrania
2.       
Yakobo
3.       
1 Petro
4.       
2 Petro
5.       
1 Yohana
6.       
2 Yohana
7.       
3 Yohana
8.       
Yuda




4.       
Kitabu cha Unabii
1.       
Ufunuo wa Yohana







Endelea kufuatilia somo linalofuata kwa uchambuzi wa kina. Share kwenye mitandao ya kijamii ili watu wapete nafasi ya kujifunza kama wewe ulivyojifunza.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAANA YA WOKOVU

Picha

HIVI NDIVYO MTU ANAVYOOKOKA

Picha

Ijumaa, 13 Desemba 2024

SOMO; MAOMBI YA KUKATAA AIBU.

SOMO; MAOMBI YA KUKATAA AIBU.

Mstari Wa Maombi; Isaya:54:4-10

Ipo hivi Unapokuwa unaishi kuna watu wako waliokuzunguka hutamani uaibike au ufedheheshwe eidha na watoto wako au mume wako au mkeo au mwenyewe kwa hiyo vita itakuwa inainuka ya kukuvunja moyo ukate tamaa au uache msimamo wa imani yako yenye ushindi uingie kukubaliana na imani inayoenda kukuangusha.

MFANO HUU;
Mama anamabint zake wanne wamesomo vizuri lakini hawaolewi na wote wazalia nyumbani kumbe ni nini kinaendelea kwenye ulimwengu wa roho imetumwa roho ya Aibu imfedheheshe yule mama na wanae katika jamii kama hataliita Jina la Yesu Kwa Moyo unaweza kushagaa wanaishi na wanaume bila utaratibu. 


Wengine aibu zinawapata makazini ofisi Zima inatambua unatembea na bosi kumbe unateswa na roho ya aibu.

Yaani mtu mwenye aibu popote akiishi atasababisha aibu tu. Hii ni roho ambayo ni mbaya mno ikikutumikisha lakini LEO Katika Maombi Utaleta heshima kama ya Rebecca  au Yaeli Wanawake waliosimama kuleta heshima mpaka Leo Tunawasoma.



MAOMBI OMBA HIVI;

Kwanza ili ujue kuomba jifunze kutamka nakufanya mazoezi ya kuomba mara kwa mara

1:Naikataa Aibu Ya Kuzaa Nje Ya ndoa nakataa Aibu Ya kuishi na Mwanaume ambaye hajafata taratibu nakataa aibu hii naikataa kwa Jina la Yesu.Amen 


2;Kila Aibu iliyotumwa juu yangu mwaka huu niipate natamka I iachie katika Jina la Yesu katika Jina la Yesu.Amen 

3:Nafuta kila Maneno ya Aibu yaliyowahi kutamkwa kwangu kwa jina la Yesu Naondoa Kila Aibu iliyotamkwa kwa wazazi wangu Katika Jina la Yesu.Amen 

4:Natengeneza Maisha ya heshima siitaki aibu kwangu Katika Jina la Yesu Naifuta Naifuta kabisa Katika Jina la Yesu.Amen 

5;Naidai heshima yangu iliyoibiwa kwa maneno au kwa macho Narundisha  Heshima yangu katika Jina la Yesu.Amen 

Endelea kutamka maneno ya kudai heshima yako nakuikataa aibu Fata mfano wa uwasilishaji kama nilivyotamka mimi.



Shirikisha ndugu zako wazazi wako nk


Kujiunga kwenye group la maombi na mafundisho nitumie ujumbe WhatsApp kwenda+255759861768

Jumanne, 10 Desemba 2024

SOMO;Maombi Ya Ulizi Usiku

SOMO:MAOMBI YA USIKU. KABLA HUJALALA

Naitwa Pastor Richard Nipo Morogoro Veta Dakawa 

Karibu Maombi Ya Kuomba ulizi Usiku Mungu Akulinde Omba hivi.


6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha Bwana, msiwe na kimya;
Isaya 62 :6


πŸ‘‰ Baba katika jina la Yesu , achilia nguvu yako , mamlaka yako,na uweza wako juu ya yule baba, mama, kaka na dada katika familia yake usiku huu katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth.Amen


πŸ‘‰Katika jina lipitalo majina yote la BWANA wetu YESU KRISTO wa Nazareth tunaagamiza kila silaha iliyotengenezwa toka kwenye ufalme wa giza  kumdhuru yule baba mama , kaka na dada pamoja na familia yake , tunawasambaratisha wote waliokaa ili kumtumia mabaya na mateso ,tunawaangamiza hata majini na mapepo na wanyama , wadudu au ndege waliotumwa kuleta mabaya wakati wa kulala katika jina la Yesu .



15 Tazama, yamkini watakusanyana; lakini si kwa shauri langu. Watu wo wote watakaokusanyana juu yako wataanguka kwa ajili yako.
Isaya 54 :15


16 Tazama, nimemwumba mhunzi avukutaye moto wa makaa, akatoa silaha kwa kazi yake; nami nimemwumba mharibu ili aharibu.
Isaya 54 :16


17 Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana.
Isaya 54 :17



πŸ‘‰ Tunaondosha kila pigo na nguvu za mauti kwa yule baba, mama, kaka , dada pamoja na familia yake katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth.


πŸ‘‰Ee roho ya Mauti , mauti ya magonjwa kwenye macho , tumbo , kichwa , masikio , kifua, moyo , milango ya uzazi , miguu , mikono , uti wa mgongo , ngozi n.k   .Tunakuamuru katika jina la,Yesu toka , achia mwili wa yule baba,mama, kaka,dada ,na familia yake na marafiki zake , roho ya mauti hutainuka tena tunakuseta kuzimu katika jina la Yesu .



πŸ‘‰Wasimamizi wa ndoto mbaya , majoka ,roho za wafu, matambiko , majeneza na makaburi imeandikwa hivi

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡


14 Nitawakomboa na nguvu za kaburi; nitawaokoa na mauti; ewe mauti, ya wapi mapigo yako? Ewe kaburi, ku wapi kuharibu kwako? Kujuta kutafichwa na macho yangu.
Hosea 13 :14

toka katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth.



πŸ‘‰Naamuru kila roho za mapepo na majini kuangamizwa kwa damu ya Yesu , ninaamuru kila nira ya magonjwa kutoweka kwenye mwili ,nafsi na roho ya yule baba mama na familia yake katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth.

27 Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani mwako, na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa, kwa sababu ya kutiwa mafuta.
Isaya 10 :27



Naitwa Pastor Richard 

Kutoka Kanisa la Holy Spirit Tanzania 

Moto wa Yesu

Morogoro Veta Dakawa 


Share 


Jumatatu, 25 Novemba 2024

SOMO:, KUTAFUTA NA KUPOTEZA UNACHOPATA HUFANYI LA MAANA

SOMO;ROHO YA KUTAFUTA NA KUPOTEZA UNACHOPATA HUFANYI LA MAANA.

Kuna Watu Wanayonguvu ya kutafuta na Kupata Pesa Lakini Hawana nguvu ya kutumia Pesa yao ikawapa faida. Hii ni roho hatari imekuwa ikitesa Watu Wengi Sana Wapo wengine Wanapata kazi mwaka mmoja Ameshapoteza Kazi Tena. Wengine wamepoteza wachumba wao wengine ndoa  zimepotea. Nk.

KUTAFUTA=Ni kujishughulisha na kitu.

KUPOTEZA=Ni kutumia ulichokipata katika mambo ambayo hayana Maana.

Karibu Naitwa Pastor Richard Nipo Morogoro Veta Dakawa Kutoka Kanisa la Holy Spirit Church  Tanzania 

        MISTARI YA KUSIMAMIA TUSOME.
  Nehemia:6:16  Isaya:44:12

            Muhubiri:3:6
6 wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza,
wakati wa kuweka na wakati wa kutupa

          Kumb.Torati:15:9
9 Jihadhari usijiwekee wazo hili ovu: “Mwaka wa saba, mwaka wa kufuta madeni umekaribia,” usije ukaonyesha nia mbaya kwa ndugu yako mhitaji na ukaacha kumpa chochote. Anaweza kumlalamikia Bwana dhidi yako nawe utakuwa umepatikana na hatia ya dhambi.


KABLA YA KUOMBA FANYA HAYA.

1:Kwanza Uwe na Utayari kuikataa hali ya kupoteza.

2;Ingia uombe hakikisha unatamka Maneno


➖"Natafuta Pesa nitazitumia Sitapoteza Pesa ikae mikononi mwangu kuanzia Leo Katika Jina la Yesu.Amen 

➖Nakataa kuwa mtumwa wa kutafuta Pesa halafu hazikai mikononi mwangu Sasa ninaamuru Pesa nitakayoishika kuanzia mwezi huu Katika Jina la Yesu.Amen 

➖Roho ya Kupoteza Achia Kazi yangu achia Uchumi wangu achia ndoa yangu achia Katika Jina la Yesu.Amen 

➖Baba Yangu Ninaomba kila kifungo kilichounganishwa ndani yangu kinifanye niwe napoteza vitu kiniachie katika Jina la Yesu.Amen 

Endelea Kuombea kila mazingira Ambayo umekuwa ukipoteza wapo wengine wanashika mimba zinaharibika Wengine Wamepoteza Afya zao Wapo wengine wachumba wamepoteza hata mawasiliano hakuna Sasa basi Shughulika Bila kuchoka hii roho ikutoke.

UTAJUAJE UMESHAFUNGULIWA.

Hutapoteza Vitu utakuwa unaona faida.
Waliokukopa watakulipa Madeni.
Utashika mimba na haitaharibika
Utafanya kazi Faida utaona.

HITIMISHO 
Unajua watu wengi mikono yao  imefungwa wanatufuta hawatumii kuleta faida katika kile walichokitafuta.
Basi Tuombe Mungu atufungue roho za kupoteza Tusiwe Tunapoteza.


Tuma ujumbe WhatsApp Uombe kuungwa kwenye group hili la maombi na mafundisho +255759861868


Jumatano, 20 Novemba 2024

SOMO; Mungu Huzingatia Haya Anapojibu.

Somo: MUNGU HUZINGATIA YAFATAYO ANAPOFANYIA KAZI OMBI LAKO.

Hakikisha hizi CV unazo kabla ya kuwasilisha Mahitaji Yako mbele Zake.

Unajua Watoto Wa Mungu Wengi na Watu Wengi Hufikiria Mungu Ukimuomba Anajibu tu hazingatii chochote Maana Wajibu Wake Kujibu. Hapana Mungu Hayuko Hivyo Mungu Yupo Makini Sana Kumsikiliza Mwanao Anapomuita Kuliko Eneo lolote Sasa ili Amjibu Katika Maombi Yake huzingatia Yafayo:
Naitwa Pastor Richard Nipo Morogoro Veta Dakawa Kanisa la Holy Spirit church Tanzania 
➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖
1:KWANZA WEWE UNAYEMUOMBA AFANYE KITU AU AKUJIBU MAHITAJI YAKO UMEFANYA NINI KWAKE..? YAANI UNAALAMA NGANI UMEFANYA KWA MUNGU?

Swali hili jiulize na ufikirie wewe unaomba Mungu Afanye hiki Wewe mwenyewe mwizi wa zaka hujawahi nunua kanisani hata Tenzi za rohoni hata viti hata kushonea watumishi suti au wajane na Yatima. Mungu Akiutazama huu moyo wa hivi Anaacha Anamtafuta mtu Ambaye hufanya kitu kwake Yeye huyo huwa Mwaminifu kujitoa kwake kusaindia wengine nk.
.
REJEA HIVI VITABU UJIFUNZE KITU.
MATENDO;10...Hii habari ya mtumishi mmoja Mkuu wa majeshi Serikalini yeye na familia yake walivyokuwa watoaji

 MATENDO;9:35.....Hii habari Ya Bint mmoja Fundi Cherehani Kipato chake cha chini lakini alikuwa mtoaji.

1Samweli:1 ....Hii Habari Ya Wazazi wake Na Samweli walivyokuwa wakijitoa kwa Bwana.

➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖

2:JAMBO LA PILI MUNGU HUANGALIA NAMNA YA UWASILISHAJI WAKO  WA MANENO.

Hatuongei ovyo ovyo Bila mtiririko Tunapoomba mbele Za Mungu  Tunapaswa Tutambue Tunaongea na Nani na Maneno Yetu Yanatakiwa Yawe ni Kiwango Kipi cha Hekima na Unyenyekevu  na Kujishusha Siyo unaongea naye Huombi mbali unalia tu au Unaenda Kwake Umenuna unaanza kumtupia lawama na kumfokea Kinywa chako kikontoro mtoto wa Mungu Usichukulie kuomba ni rahisi rahisi mpaka ulete majibu.

VITABU REJEA 
Soma Habari Ya Hanna alipokuwa Anaomba 
1Samweli:1:12-20

Soma hata Mitume Walivyokuwa wakiwasilisha maneno wakiwa wanaomba
Matendo:1:23-26

WAKOLOSAI;2:1-5
1;Nataka mjue jinsi ninavyojitaabisha kwa ajili yenu na kwa ajili ya wale walioko Laodikia, na pia kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona mimi binafsi..

 2 Kusudi langu ni watiwe moyo na kuunganishwa katika upendo, ili wapate ule utajiri wa ufahamu mkamilifu, ili waijue siri ya Mungu, yaani, Kristo mwenyewe

, 3 ambaye ndani yake kumefichwa hazina zote za hekima na maarifa.

 4 Nawaambia mambo haya ili mtu yeyote asiwadanganye kwa maneno ya kuwashawishi. 

5 Kwa kuwa ingawa mimi siko pamoja nanyi kimwili, lakini niko pamoja nanyi kiroho, nami nafurahi kuuona utaratibu wenu na jinsi uthabiti wa imani yenu katika Kristo ulivyo.


3:UKAAJI WAKATI UKIWA UNAOMBA MUNGU.

Umekaaje Kaaje Unapokuwa Unaomba Au Wewe unajua kukaa tu. Lazima ujifunze ukaaji wako ukiwa unaomba kaa kwa nidhamu na kwa heshima Sababu unaenda kuzungumza na mwenye umri kukuzidi Elimu kakuzidi Uchumi kakuzidi kila kitu Amekuzidi Kwanini ukose Adabu. Wapo watu wanapoomba ukaaji wao utafikiri hawapo kwenye kuomba Anaomba huku Ameshika hiki mara amekaa ovyo. Kama umepiga magoti piga kwa heshima. Kama ni kusimama simama kwa heshima.

REJEA KUSOMA;
➖➖➖➖➖➖➖
Matendo:20:36-38

DANIEL:6:10
 10:Basi Danieli alipofahamu kuwa amri ile imetangazwa, alikwenda nyumbani kwenye chumba chake cha ghorofani ambako madirisha yalifunguka kuelekea Yerusalemu. Akapiga magoti na kuomba mara tatu kwa siku, akimshukuru Mungu wake kama alivyokuwa akifanya mwanzoni. 


HITIMISHO 

Acha Niseme Kwamba Ni Muhimu Sana Kujua hili Sababu Unaweza Ukawa Mtu wa Kuomba maombi Yasiyo na Matokeo ikafikia hatua ukaanza kumlaumu Mungu wetu nakuona kama Anaubanguzi Anajibu Wengine kumbe wewe mwenyewe upo nje ya Kanuni Zake Mungu katika Eneo la Maombi.

Kama upo nje ya Group la Maombi na Mafundisho mtumie ujumbe WhatsApp Pastor Richard Akuunge +255759861768


Shirikisha ujumbe huu kwa kuutuma kwa watu wengi zaidi mpaka umfikie Anayependa Kumlaumu Mungu hamjibu.

NAKAMA UNAFANYA HAYA MUNGU HAJAJIBU ELEWA NI LA MUDA LAZIMA AJIBU SABABU UNAALAMA KWAKE UNAFANYA VITU NA KUJITOA KUSAPOT KAZI YAKE HAUFURAHII UKIONA INATUKANWA AU WATUMISHI WAKE WAKILALA NJAA UNAJITOA KUWALISHA.

Jumapili, 3 Novemba 2024

SOMO:MAOMBI YA KUOMBEA HAJA YA MOYO WAKO

            "DARASA LA MAOMBI "
=============================
SOMO:MAOMBI YA KUOMBEA HAJA YA MOYO WAKO.

Kila mtu huwa Anamatamanio Ya Vitu Anataka Avipate Lakini Hawezi Kuomba Akavipata Sasa Kupitia Darasa hili la Maombi utajifunza uombaje

MUNGU HUZINGATIA 
1;Uwasilishaji wa Maneno.
2;Ukaaji na Uaminifu Wako kwake.
Hakikisha hivi vitu uwe navyo ukitaka unaomba unaleta majibu.

Naitwa Pastor Richard Nipo Morogoro Veta Dakawa 

Tunasimamia Mistari hii.Tusome.
        MITHALI;30;7-8
7 “Ninakuomba vitu viwili, Ee Bwana;
usininyime kabla sijafa:

8 Uutenge mbali nami udanganyifu na uongo;
usinipe umaskini wala utajiri,
Bali unipe chakula cha kunitosha kila siku

MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOOMBA;

1:Omba Kitu Ambacho ukikipata hutamuacha Mungu Sababu kuna Vitu vingine ukivipata tu Wewe Vinakutenga na Mungu.

2;Omba Kataa Umasikini na Kila hali inayofanya Watu Wakudharau.

3:Omba Uwe na Upendo Wa Kiasi kwa Kila Eneo.


NAMNA UTAKAVYOOMBA;

MFANO : 1:UNAOMBA UOLEWE/UOWE.

πŸ‘‰Bwana Wangu Mwokozi Wangu Umenijua toka tumboni mwa mama ukanipima uaminifu wangu kwako katika utoaji wa zaka Na Sadaka Nimekuwa mwaminifu pia hata dhambi ya kuzini nimeishinda Bwana Wewe Mwenyewe Unaona Nilivyosimama Kujitunza Nipate Kibali Machoni Pako Mungu Wangu Niletee Mume Wangu Ubavu wangu au Niletee Mke Wangu Nyama katika mifupa yangu Muda wa Mimi Kuwa na Mwezangu umefika mfungulie Miguu Anifate Katika Jina La Yesu.Amen 

Rudia ×6
ANGALIZO:
Hakikisha Unapoomba uendane na maneno yako uwe kweli zaka umesimama mwaminifu uwe kweli huzini. Mungu huwa hajibu kwa mtu asiyemwaminifu kwake.


MFANO 2; UNATAKA UPATE KAZI.

Baba Yangu Bwana Mwenye nguvu na Mamlaka Nashukuru Kwa Nafasi hii umenipa nione Nami Napendwa nawewe nimeomba kazi Baba Nimeomba Kazi Baba Naomba Jina Langu Lisikosekane Jina langu mimi mwanao Ni Richard Julius Kushoka Ndiyo hivyo nimejaza kwenye usaili Tuma Malaika Wako hili Jina Walipitishe Kila Eneo litapoonekana nami nakuapia Mungu nikipata Kazi Nitakuwa Mwaminifu Sana Tena Sana Kwenye hii Madhabahu Ya Moto Wa Yesu.Amen 

Rudia ×3
ANGALIZO:
Hakikisha Ukipata Kazi Huachi Kutoa Fungu la Kumi Unakuwa Mwaminifu kupita Kawaida.


MFANO;3 KUOMBA UWE NA UZAO YAANI UPATE WATOTO.

πŸ‘‰Shika Tumbo lako Ongea maneno haya kwa mwanamke.

Wewe Tumbo Nakuongelesha uliambiwa nikiolewa tu ulete Uzao Uijaze Dunia ulete Watoto Kwanini mpaka Sasa huna uzao Nakuamru kama kuna anayekuzuia au Amekufunga usinipe watoto nakufungua kwa Jina la Yesu. AMEEN 


πŸ‘‰Mwanaume Shika Kiuno Kama Huzai.

Wewe Kiuno changu Nakuambia kuanzia Sasa ufunguke ukazalishe Mbengu zilizopo ndani yangu zitungishe mimba kila kinachozuia mimi nisiitwe Baba Kiachie Katika Jina la Yesu.Amen 

Rudia ×1
ANGALIZO:
Hakikisha unatamka nilivyoelekeza Kwa kila jinsia omba mara kwa mara sio uombe siku moja tu.


MFANO:4 KUOMBA UPATE MTAJI WA BIASHARA 

πŸ‘‰Bwana Yesu Nakuomba uwaruhusu watu uliowadaa wanipe mtaji waje nimechoka kukaa bila kukutolea zaka najiona kama ni mwenye hatia nipe mtaji Baba Uone uaminifu wangu nitakavyosimama kuwa mwaminifu pia unipe na wateja wengi Sana. KATIKA Jina la Yesu Ameen 

        OMBEA WATEJA;
Baba Yangu fungulia Wateja muondoe kwenye mlango pepo anayezuia wateja wasiingie Bwana Weka Malaika wako Awe Anawavuta Wateja Waje waje Waje Kwa Wingi Katika Jina la Yesu.Amen 

ANGALIZO:
Kila uendapo kwenye biashara ombea upate wateja wengi.

MFANO:5 OMBEA MAHITAJI YAKO MBALIMBALI.

Mahitaji yapo mengi Kwa hiyo Ni Vyema Zingatia Uwasilisha wa maneno yako Kwa Mungu unapoomba pia kuwa mwaminifu kwa Mungu acha kuwa mdanganyifu kwa Mungu.

Mfano:Kuomba upone magonjwa;
Baba Yangu Nakuomba niondolee magonjwa mwilini mwangu Baba nitazame mwanao kwa jicho la huruma nipo chini ya miguu yako kwanini unaruhusu magonjwa mwilini mwangu kumbuka nilivyomwaminifu katika madhabahu hii ya Moto wa Yesu sijawahi kuacha kukutolea Zaka na hii ndiyo Madhabahu uliyonipa Bwana Kumbuka nimenunua vyombo vya mziki kanisani nimenunua viti yote hii ni uaminifu na Upendo wangu kwako Baba Kumbuka niliyoyafanya kwako naitaji niendelee Kufanya Nakuomba Uniondolee mateso haya mwilini mwangu Baba nitafanya kwako zaidi ya niliyoyafanya kwako Ansate Mungu umesikia Maombi Yangu Nipe nguvu Sasa kwenye mifupa yangu Mwili wangu nitembee nifanye kazi zangu pasipo na magonjwa nikienda Hospitali wasione tatizo tena nafunga kabisa kwa Jina la Yesu.Amen 

Rudia ×5

ANGALIZO 
Hakikisha unapoomba uwe kuna vitu unafanya kwa Mungu iwe kama Sababu ya Mungu Akuponye ili uendelee kufanya mengi kwake kama huna Sababu ni ngumu sana kumshawishi Mungu.
Kumbuka Ezekiel alifanya kitu Akaponywa magonjwa.



Natumaini Kuna Jambo umejifunza Naomba ukiwa unaswali niulize inbox WhatsApp number +255759861768

Shirikisha wengine


Jumanne, 1 Oktoba 2024

MAOMBI YA KUITA MWILI WAKO ORIGINALLY USIO NA MATESO NA KUONDOA MWILI

SOMO; MAOMBI YA KUITA MWILI WAKO ORIGINALLY USIO NA MATESO NA KUONDOA MWILI  FAKE UNAOTESEKA.

🀲🀲🀲🀲🀲🀲🀲🀲🀲🀲🀲🀲🀲
Ndugu Yangu Katika Ulimwengu Wa roho hauwezi kuutesa mwili au kuufunga mwili original wanachokifanya Adui Zako Wanachukua Nafsi yako na Mwili Wako Wanaleta Mwili Fake Katika Muonekano wa roho lakini Katika Damu na nyama utaona ule ule kumbe siyo.

Mfano: Mtu Anaendeshwa na madeni magonjwa mwilini Pake Hayaishi mapepo hayaishagi Ameombewa Sana Kumbe Sababu Unaombea Fake original Anakuwa yupo kuzimu.


TAFADHALI SOMA KWA UMAKINI MANENO HAYA TAFAKARI.

          "1 Timotheo 5:6  
Bali, yeye asiyejizuia nafsi yake amekufa ingawa yu hai.

Kumbe Unaweza ukaona Umekufa kumbe upo hai unaona unamagonjwa kumbe originally haumwi.


            Yohana 11:14, 39-43
14 Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

39 Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne.

40 Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?

41 Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia.

42 Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma.

43 Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje.

HII MISTARI TUNAJIFUNZA KITU YESU ALIVYOMFUFUA LAZARO.


Maombi Ya Bwana Yesu Kuuita Mwili Alitaja mambo matatu.

1;Jina la Aliyekufa

2:Akatumia Neno "NJOO"

3:Uchungu na Kuugua Moyo Kuona Mzingo.

Yesu Aliona Mzingo ndiyo Maana Alimwita kwa Uchungu.


MAOMBI HAYA TUNAVYOPASA KUYAOMBA.

Soma hii mistari ya Ushindi Kabla Hujaomba
.
        Zaburi 118:17 
 Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana.
"""""::::::"""""......""""""......."""""".......
       Zaburi 118:19-20
19 Nifungulieni malango ya haki, Nitaingia na kumshukuru Bwana.

20 Lango hili ni la Bwana, Wenye haki ndio watakaoliingia.
πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡
Zaburi 35:1-6
1 Ee Bwana, utete nao wanaoteta nami, Upigane nao wanaopigana nami.

2 Uishike ngao na kigao, Usimame unisaidie.

3 Uutoe na mkuki uwapinge wanaonifuatia, Uiambie nafsi yangu, Mimi ni wokovu wako.

4 Waaibishwe, wafedheheshwe, Wanaoitafuta nafsi yangu. Warudishwe nyuma, wafadhaishwe, Wanaonizulia mabaya.

5 Wawe kama makapi mbele ya upepo, Malaika wa Bwana akiwaangusha chini.

6 Njia yao na iwe giza na utelezi, Malaika wa Bwana akiwafuatia.


UTAOMBA HIVI 

Ita Mwili original kataa mwili wa magonjwa mateso nk

1●ITA MWILI WAKO ORIGINALLY 
Utatamka maneno haya.
Naita Mwili wangu original njooo fake Ondoka kwenye maisha yangu

Mwili wangu hauna magonjwa mwili wangu hauna Vifungo Mwili Wangu Upo huru Nina Afya Nina Amani Ondoka Mwili Fake Kwa Jina La Yesu Mwili wangu usio na madeni mawazo yangu moyo wangu Narundisha kila kitu kilichofake kiondoke katika Jina la Yesu

Rudia mara nyingi zaidi uwezavyo.pia Kila hali ya maisha hiyo ni fake kataa lete original.

.2:●KIRI KUMKATAA FAKE NA MWILI WAKE.

Nakiri kuukataa huu mwili Siyo wangu ninachojua mwili wangu original hauna magonjwa mwili wangu original hauna vifungo Ninautaka mwili huo kwa Jina la Yesu Sitaki Sitaki Sitaki mwili wenu katika Jina la Yesu.Amen. 


Nakiri Kwamba hofu hii siyo yangu mawazo haya ya kukubaliana mateso yenu au vifungo siyo mimi nimekataa original ninakataa kuteswa mliponifungia mniachie.


3:●ORIGINALLY AJITAMKIE USHINDI.

Mimi mwili Original Ninatambua Nipo huru na Kila Kifungo chenu roho ya kunifunga nisiolewe au nisiowe nasema nitaowa au kuolewa kila Eneo langu mlilorithisha kuzimu nasema kwamba hamtaweza mimi mwili original 
Nina Imani ninavuka nakuvusha wengine Sina hofu wala siongopi Sina magonjwa Sina vifungo 

Endelea Kukiri Kukataa Yale Unayapitia Sababu wewe ni Original. 

Tembea Tembea ndani kwako 

4●FUNGA WALIZI WALIOLINDA MWILI ORIGINALLY ASIJE KWENYE MWILI WAKE.

Natamka Kuanzia Leo mwili Original Hautaondoshwa Tena Umerundi mifupa yangu imerundi mawazo yangu yamerundi Katika Jina la Yesu.Amen 



5●MSHUKURU MUNGU 

Nyosha mikono Juu Piga makofi Kiri mwili uliofunguliwa usio na vifungo MSHUKURU  Mungu Kwa Ajili ya Pastor Richard Kumfunulia haya Maombi Mshukuru Mungu Kwa Ajili Ya Kukutenga Na mwili Fake kuurundisha mwili wako.
Piga makofi ukimtukuza Bwana


HITIMISHO 

Haya ni mambo ya rohoni Sana ni ngumu kujua Kama Bila Roho huwezi kujua unaweza kug,ag,ania kuomba Kumbe unashughulika na mwili fake.


Wito
Chochea Kuomba fanya mazoezi ya kuomba mara kwa mara

WhatsApp Pastor Richard +255759861768

Share



MAOMBI YA USIKU WA MANANE MWEZI OCTOBER '------DECEMBER 2024

SOMO: MAOMBI YA USIKU WA MANANE OCTOBER____DECEMBER 2024

Karibu Katika Msimu WA  Mwisho WA Maombi Ya Usiku Wa Manane Kwa Mwaka 2024 Ambao Ni Mwaka Wa Kusitawi 
Mwanzo 26;13

TUMEONA SHUHUDA WATU WENYE MIAKA 52 WANAOLEWA KUPITIA MAOMBI YA USIKU WA MANANE 

TUMEONA WASIO NAKAZI WANAPATA KAZI

TUMEONA WATU WENYE MIAKA 48 WANAZAA

TUMEONA WENYE VIFUNGO MBALIMBALI WANAFUNGULIWA KATIKA MSIMU ULIOPITA.


MAOMBI YA USIKU WA MANANE PEKEE YANAWEZA KUKUFUNGUA VIFUNGO VYAKO

AMKA SAA SABA USIKU OMBA MPAKA SAA TISA PUMZIKA


NAMNA TUTAKAVYOOMBA.

Soma Mistari 

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

1:●ANZA NA TOBA.

Zaburi;86:5  2Nyakati:7:14-16

Piga magoti mbele ya kitanda

"Baba Nakuja mbele Zako mimi mwanao Richard Nimekukosea mengi kuanzia January mpaka Sasa nimezini kimawazo nimeimba kimawazo nimeshindwa kutii maangizo ya Baba yangu wa Kiroho nimekuwa ni mwizi Na ninajiona Kabisa mambo hayaendi lakini nakuja kugundua ni sababu ya wizi wa zaka Malaki;3;8-9 Nisamehe  Nisamehe Bwana Nisamehe Bwana ninatubu maovu yangu na Dhambi Zangu Katika Jina la Yesu.Amen 🀲🀲


2;●KUKIRI USHINDI KWA KUTUMIA NENO 
.mfano huu kama ninavyoonesha.

Kuna Wakati Kiri Ushindi Siyo Kukiri mapepo au kusikiliza Sauti Za Mapepo roho za kushindwa.

1;Sitaki kutumikia Vifungo au Magonjwa mimi "Nataka Nimtumikie Bwana" Kutoka:23;25


2;Sitaki Kuitwa Tasa mimi au Kuharibu mimba "Nataka Nizae watoto siyo mtoto".
Kutoka:23:26

3;Sitaongopa Adui Zangu" Kuanzia Leo nitakuwa na Utisho Mkubwa Kila Adui yangu Ataniongopa" Kutoka;23:27

4:Sitaongopa kwa kuwa "Bwana ni ngome yangu atawarundishia mabaya yao"
Zaburi;94:22-23

5:Sitaacha Kutoa zaka" Nitakuwa mwaminifu kwa Bwana ili Anibariki umasikini siutaki"
Kumb.Torati:28:1

6:Sitaumwa Tena Maana "Mungu Amenirundishia Afya Yangu"
Yeremia:30:17

7:Sitaki Kuwa mnyonge tena "Nakata Unyonge Ndani Yangu Kuanzia Leo"
Wafilipi:3:21 Zaburi:136:23


HAKIKISHA UNASOMA HIYO MISTARI YA BIBLIA NA KUITAFAKARI.


3●JITABIRIE BARAKA MWENYEWE.

1;Mwezi huu Mimi nitaolewa na nitatolewa mahali au mwezi huu mimi nitaowa na nitafunga ndoa kabisa.



2;Maombi ya kazi niliyotuma naenda kupata kazi majina yakirundi na langu lipo 


3:Mkuu Wangu Atanipandisha cheo na mshahara wangu utapanda juu niweze kutia Zaka nzuri.

4;Nitajenga mwezi huu nitashusha tofali kwenye kiwanja changu au nitanunua kiwanja mwezi huu.

5;Mimi na Mchumba wangu Tutaowana mwaka huu


Endelea kujitabiria MWENYEWE kama mfano huu nilivyokuanzishia



4●SHUKURU MUNGU AMEJIBU.

Nyosha mikono juu Inuka simama piga makofi mara nyingi Sema Nashukuru Mungu kwa Kujibu ombi langu Nashukuru Nashukuru Nashukuru Mungu Sana Pokea Sifa na Utukufu wako Katika Jina la Yesu.Amen 

5:●FUNIKA MAOMBI YAKO KWA DAMU YA YESU

Nayafunika maombi Yangu Kwa Damu Ya Yesu Nakuomba Bwana Uyazungukie kwa ulizi wako Katika Jina la Yesu Ameen 


BAADA YA KUMALIZA FUNGUA AUDIO  YA MAOMBI NILIYOTUMA UGANISHA NA RADIO SAFIRI NAMI KATIKA MAOMBI 

Huu Utaratibu Tunaenda nao Mpaka December Tutaanza Kujiandaa nauli ya kutufikisha Morogoro Veta Dakawa Kuja kufunga mwaka Pamoja Tar 30 Tunaingia Makao makuu kuja kufunga mwaka huu wa kustawi 2024 Nakuingia Mwaka tutakaopewa Jina. Uje na Sadaka yako ya kufunga mwaka Tunakuwanga na Maombi moto moto Sana Usikose.

Naitwa Pastor Richard Nipo Morogoro Veta Dakawa 

Askofu mkuu wa makanisa ya Holy Spirit church Tanzania 

Simu +255759861768

Ijumaa, 27 Septemba 2024

MSINGI IMARA WA NDOA

          SOMO; MSINGI IMARA WA NDOA 

Naitwa Mwalimu wa Wanandoa Pastor Richard Kutoka Kanisa la Holy Spirit church Tanzania 
Msingi Wa Ndoa Huanzwa Kujengwa Kwenye Uchumba Kabla hata hujampata mtu wako Sahihi Isaka Anasema Wakati Anamtafuta Rebeca Akaweka Vingezo Au Sifa Ya Kile Anachokitaka. Hicho ndicho kilichowaunganisha Rebecca na Isaka Vingezo alivyo navyo Rebeka Wengine hawakuwa navyo.

1;MSINGI WA KWANZA ANASIFA TOFAUTI NA WENGINE NDIYO MAANA UMEMPENDA.
Mwanzo;24 Habari ya ndoa ya Isaka.

Mwanamke au Mwanaume Mpaka Unakubali kuolewa au Kuowa ukafunga ndoa umemuona Anasifa tofauti na Wanawake Wengine heshimu hilo na ulinde na kutunza siyo siku mbili tu umeanza kuona Sifa zile hana umeanza kutamani wengine.


2:MSINGI WENU WA PILI; RUHUSU MUNGU MWENYEWE AWE MJENZI WA NDOA YENU.

Mnapoyapa nafasi maombi na Ibada Kwenda Kanisani kuomba kuombea malengo yenu na Kuwa Waaminifu Wa Fungu la Kumi  Mnamfanya Mungu Aijenge ndoa Yenu Vizuri Tena Kwa Upendo  

SOMA HII MISTARI;
             Zaburi:127;1
Bwana asipoijenga nyumba Waijengao wafanya kazi bure. 

       2 Wakorintho 3:17 
 Basi ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru.
===========================/

2:WAPENDENI NDUGU ZENU PANDE ZOTE MBILI;
Wakija ndugu kuwatembelea Unaweza ukaandaa kasupu kawasaki na Vinyard vya kukaaga mama wake zako unawakaribisha huku unajiongelesha yani huku mboga za shida Tumeamua tuwaandalie hii Mboga Mtusamehe tu. Wanawishe kwa heshima hapo.

     SOMA MISTARI HAYA:
             Warumi 12:10-15
10 Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu;

11 kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;

12 kwa tumaini, mkifurahi; katika dhiki, mkisubiri; katika kusali, mkidumu;

13 kwa mahitaji ya watakatifu, mkifuata ukarimu; katika kukaribisha wageni mkijitahidi.

14 Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani.

15 Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao.

===========================

3:MSHIRIKIANE NA JAMII INAYOWAZUNGUKA MFANYIKE BARAKA KWA JAMII:

Shirikiana Na Jamii Katika Mambo Ya Msingi Ambayo hayakutengi na Mungu wako kama msimba maendeleo na Harusi mbalimbali nk unapokuwa umepewa taarifa.

      Mithali 1:14-16
14 Wewe utashirikiana nasi; Tutakuwa na vitu vyote shirika.

15 Mwanangu, usiende njiani pamoja nao; Uzuie mguu wako usiende katika mapito yao.

16 Maana miguu yao huenda mbio maovuni, Nao hufanya haraka ili kumwaga damu.

=================================

4:LINDENI HESHIMA YENU.

Jamii inayowashuhudia kwenye tukio la ndoa ambalo Tunalitaja Kuwa la heshima hiyo hiyo jamii itakuja kuwashagaa Mkija Kufanya mambo ya Ajabu.

Mfano; Mkaanza Kupigana Au Kunyanyasa watoto wenu mtakaobarikiwa nao.

Kosa lingine lipo kwa Mwanandoa Akaanza kumpa nafasi za mke wake mwanae mfano ukipata pesa mwanao ndiyo unamkabidhi mkeo anamuomba mwanao au kwenda kulala chumbani kwa mwanao Hii inaondoa heshima Sana.

MISTARI YA KUSOMA

         Zaburi 111:3-5
3 Kazi yake ni heshima na adhama, Na haki yake yakaa milele.

4 Amefanya ukumbusho wa matendo yake ya ajabu; Bwana ni mwenye fadhili na rehema.

5 Amewapa wamchao chakula; Atalikumbuka agano lake milele.

=================================


5:MIOYO YENU IFUNGUKE NA KUWEKANA WAZI USIYOYAPENDA NA UNAYOYAPENDA.

Hakikisheni Tabia Ambazo Unaziona Zinataka Kuingia kwa Mwezako Unakaa naye chini Kwa Utaratibu Na Kwa Heshima muulize Tu Kwanini Anafanya Kitu Ambacho Ulishamwambia Hupendi Pia Mweleze Wewe Unapenda hiki na hiki.
===============================
MISTARI YA KUSOMA

          Mithali 17:26-28
26 Tena kumwadhibu mwenye haki si vizuri; Wala si kwema kuwapiga wakuu kwa unyofu wao.

27 Azuiaye maneno yake ni mwenye maarifa; Na mwenye roho ya utulivu ana busara.

28 Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima; Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.
==============================

6:MALIZENI TOFAUTI ZENU NYINYI WENYEWE.

Kila Mnapokuwa mmetofautiana Au Kugombana Mnatakiwa Mmalize Tofauti Zenu Wenyewe bila kuzitoa nje. Msifanye Tofauti Zenu Zikafikia Hatua Zikawa Kubwa mpaka mkashindwa kuzitatua.
=======÷==========÷÷÷÷÷÷==========
MISTARI YA KUSOMA 
     Wakolosai 3:13-17
13 mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.

14 Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.

15 Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.

16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.

17 Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.


7:CHANGUENI WALEZI WA NDOA  YENU WALIOKAA MUDA KWENYE NDOA 

Sifa za Mlezi wa ndoa 
a)Awe Amedumu kuanzia miaka 3 Nakuendelea

b)Awe na Hekima na Busara

C)Awe Mwenye Kuingwa na Mfano wa ndoa yake.

          Mithali 11:14 
 Pasipo mashauri taifa huanguka; Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.


8;Kila Mmoja Aufundishe Moyo wake Kupenda na Kuongea maneno ya Hekima .

Nyinyi ni Wanandoa Mnatakiwa Kupendana na Kuvumiliana Kila changamoto mtakayokuwa mnakutana nayo.

     ⁶Yohana 13:34
 Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.


9:MANENO MATATU YENYE USHINDI 

1:Vumilia Katika Kila Kipindi

     1 Petro 2:19  
Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki.

2:Usiongope changamoto za Kwenye ndoa

          Yeremia 1:8 
 Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana.

3;Amini Kila Jambo linasababu yake.

            Mhubiri 3:1 
 Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.


10;MAFANIKIO NA UPENDO NDANI YA NDOA

MAFANIKIO HUJENGWA NA VITATU HIVI;

1;MUNGU AWE NAMBA MOJA.
Msifanye jambo lolote bila kumhusisha Mungu.

2;MKEO AWE NAMBA MOJA .
Usifanye kitu chochote bila kushauriana na mkeo

3:MUME AWE NAMBA MOJA.
Usifanye Kitu chochote bila kushauriana na mumeo.


UPENDO HUJENGWA NA VINNE.

1;Tumia Neno la "NAKUPENDA" lifelike kwa mwezi wako mara kwa mara 
Muite majina mazuri mazuri Hanny Sweet My love mke wangu mume wangu nk

2:Tumia Neno "SAMAHANI" kila mnapokoseana au kwenda tofauti  tumia neno Samahani mume wangu.


3:Tumia Neno "ANSATE" kila unapoletewa kitu au kupewa kitu na mwezi wako.

4:Tumia Neno "POLE" Kila Unapomuona mwezako ametoka kazini au chochote Kile Kinachoonesha neno hili litumie.



Nataka Kusema Ndoa inajengwa na nyinyi wawili na wawili nyinyi mnaweza Kuivunja ndoa  Lindeni Agano hili mnalolipokea leo liwe mfano wa Kuingwa kwenye mioyo Yenu..


@Naitwa Pastor Richard Nipo Morogoro Veta Dakawa 
Kanisa la Holy Spirit church Tanzania 




Kanuni 10 za Uchumba

Jumamosi, 14 Septemba 2024

SOMO;MADHARA YA KUCHEZEA AGANO LA NDOA

SOMO: MADHARA YA KUCHEZEA AGANO LA NDOA.

Kuna watu wamekuwa wakichukulia kuowa au kuolewa ni kama mchezo fulani Ambao utaenda madhabahuni  unaapa na kufungishwa ndoa baada ya muda Anavunja uaminifu au ndoa kimya kimya Tena Anaenda kuolewa au kuowa pasipo kupeana Talaka kisheria Hii huwa hatari kuliko hata ugonjwa mtu anaweza kutibiwa.


1:Madhara utakayoyapata usipompa talaka kwa kosa la uzinifu au hana nguvu za kiume au nguvu za kike. Hili kosa uwe na Ushahindi umeona mwenyewe mwezako anatatizo hili ukienda kinyume eidha kwa sababu zingine nje na hizi utakuwa umeivunja ndoa mwenyewe na utateseka mno tena sana kuliko ulivyodhania.


2:Ndoa Isiyo na maelewano Takiribani ni mwaka mmoja ndani ungomvi hii inavunjika kwa sababu mnaweza kuja kuuwana ni bora mkatengana lakini Hampigani mnanuniana tu ukataka ndoa uvunje itakutesa sana.

3:Hurusiwi Kuivunja ndoa ikiwa hata mwaka haijamalizika ukifanya hivyo utaadhibiwa kimaisha Utatembea na laana isiyofutika.


4:Hutakiwi Ndoa yako uivunje kienyeji ukarukia moja kwa moja mahakamani bila kuanza huku chini kwa msajili wa ndoa nikosa kubwa Sana Usipofata utaratibu hiyo laana itakutesa milele.


5;Msajili Akisema hapana hata mbele huku hutakumbalika maana hamkukaa ulijiamulia tu hakikisha unafata utaratibu wa kisheria unapotaka kuvunja ndoa.


6:Ndoa inaweza kuvunjwa na hawa wawili wakawa huru lakini siyo rahisi rahisi sababu ambazo hazina mashiko.

Kwa Mungu Inamuonya huyu mtu anayeingia Kwenye ndoa Baada Ya Muda Anadai ndoa ivunjike chezea vyote usije ukacheza na Agano la ndoa

Tunasoma
Marko 10:9 
 Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.



HITIMISHO 

Ndoa inaitaji ilindwe na watu wote ikiwemo nyinyi Wanandoa Ndoa Siyo fashion

Jumatatu, 9 Septemba 2024

MAOMBI YA KUOMBA KUFUNGUA KIZUIZI



        DARASA LA MAOMBI 

SOMO: MAOMBI YA KUFUNGUA KIZUIZI.

Ukiona Unataka ufanye kitu kinaingilia kitu kilichokuwa haikipo kwenye hesabu zako ujue hizo ni Vizuizi.
Mfano; Unanyumba Unauza Wateja wanafika pale mnapanga bei gafla wakirundi wanasema hawanunui ujue kuna Kizuizi.

UNACHOTAKIWA UOMBE SASA.

Utafata hivi ninavyoelekeza 

KWANZA TAFUTA MSTARI 

Tunasimamia:
Marko 3:27 Hawezi mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu, na kuviteka vitu vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu; ndipo atakapoiteka nyumba yake.

"Baba Nasimama Sawasawa  Na Neno lako Katika Kitabu cha Marko:3:27 Namuondoa huyo Mtu Anayenizuia Mimi Au Kuweka uchawi wake wa Kunirundisha nyuma Kwa Jina la Yesu Navunja vipande Magongo na Kamba Zilizofunga hili swala langu la ndoa au Kiwaja au Kazi nisipate Kwa Jinaa la Yesu Fuguka Fuguka fuguka kwa sasa nakuendelea sitaki kuwa mnyonge Kuanzia muda huu nitakuwa na nguvu na nguvu kweli kweli Ninaomba Kwa Imani ya Jina la Yesu.Amen 

RUDIA ×8 KUOMBA

Kama Hujaungwa Kwenye Group la Maombi na Mafundisho mfate WhatsApp Pastor Richard Akuunge +255759861768 Utajibu maswali kabla hujakubaliwa kuwa mwanangroup


Jumamosi, 7 Septemba 2024

Maswali na majibu Jumapili.9/9/2024

   DARASA LA
BIBLIA MASWALI NA MAJIBU  

Karibu katika Kipindi Kipya kitakakuinjia kwenye Group letu la Maombi Kila Jumatatu Asubuhi Lengo Ni Wewe Kuendelea Kuzidi kujifunza Maswali na Majibu mbalimbali 
Hakikisha unaandika maana usije ukaniambia nirushe swali ambalo lilishapita kuanzia Leo Anza Kufatilia.
Naitwa Pastor Richard 

TUMEANZA NA HAYA MASWALI:    

 Swali:1
Nini Kitanizuia nisibatizwe kwa maji mengi..?
Ni kitabu ngani kinasema hivyo na Ni nani aliyesema maneno hayo..?

Jibu;Matendo;8:36

              Swali:2
Biblia haikuandikwa mambo yote ingeandikwa kitabu kisengetosha..?
Kitabu ngani kinasema  maneno haya.
A.Mwanzo
B.Hesabu
C.Luka
D.Yohana 21:25✅
E.Zaburi.

             Swali: 3
Utatu mtakatifu ulifunuliwa au ulitambulishwa lini kwetu mpaka Tukaujua..?

Jibu;Kipindi cha Ubatizo wa Yesu. 
Mathayo;3;16-17


       Swali:4
Swali la Kwanza Toka Dunia iumbwe  liliulizwa na nani..? Aliliuliza Akiwa  Wapi..?

Mwanzo:3:1



MASWALI NA MAJIBU JUMAPILI TAR.15/9/2024

🌳🌳🌳🌳🌳🌳🌳🌳🌳🎈
SWALI;1

1:Yesu alipoletwa Hekaluni akiwa mtoto mchanga, ni nani aliyemtambua kuwa ndiye Masihi?

Jibu: Simeoni ( Luka 2:22-38 ).


SWALI:2

2. Ni mgombea gani ambaye hakuchaguliwa kwa wadhifa wa mtume baada ya Yuda Iskariote kujiua, kulingana na Matendo ya Mitume?

Jibu: Yusufu Barsaba (Matendo 1:24–25).


SWALI:3

3. Ni vikapu vingapi vilivyobaki baada ya Yesu kuwalisha wale 5,000?

Jibu: Vikapu 12 (Marko 8:19).


SWALI:4

4. Katika mfano unaopatikana katika Injili tatu kati ya nne, Yesu alilinganisha mbegu ya haradali na nini?

Jibu:  Ufalme wa Mungu ( Mt. 21:43 ).


SWALI:5

5: Musa alikuwa na umri gani alipokufa, kulingana na kitabu cha Kumbukumbu la Torati?

Jibu: Miaka 120 (Kumbukumbu la Torati 34:5-7).


SWALI:6

6: Ni kijiji gani kilikuwa mahali pa kupaa kwa Yesu, kulingana na Luka?

Jibu: Bethania ( Marko 16:19).


SWALI:7

7. Ni nani anayefasiri maono ya Danieli ya kondoo mume na beberu katika Kitabu cha Danieli?

Jibu: Malaika Mkuu Gabrieli ( Danieli 8:5-7 ).



TAR.22/9/2024 JUMAPILI 


SWALI:88:Ni yupi kati ya mke wa Mfalme Ahabu, aliyetupwa kutoka dirishani na kukanyagwa kwa miguu?

Jibu: Malkia Yezebeli (1 Wafalme: 31).



 

 Nifanye nini ili niokolewe?

  •  Unapaswa kuamini kwamba Yesu alidhabihu uhai wake kwa ajili ya dhambi zetu. (Matendo 16:30, 31; 1 Yohana 2:2) Hilo linamaanisha kuamini kwamba Yesu alikuwa mtu halisi na kwamba mambo yote ambayo simulizi la Biblia linasema kumhusu ni sahihi.

  •  Jifunze kile ambacho Biblia inafundisha hasa. (2 Timotheo 3:15) Biblia inasema kwamba mtume Paulo na Sila walimwambia hivi mlinzi wa jela: “Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokolewa, wewe na watu wa nyumba yako.” Kisha, baada ya hapo, walianza kumfundisha mlinzi huyo wa jela “neno la Yehova.” a (Matendo 16:31, 32) Hilo linaonyesha kwamba mlinzi huyo wa jela hangeweza kumwamini Yesu bila kuwa na ujuzi wa msingi wa Neno la Mungu. Alihitaji kuwa na ujuzi sahihi wa Maandiko.—1 Timotheo 2:3, 4.

  •  Tubu. (Matendo 3:19) Pia, lazima utubu, au uhuzunishwe sana, kuhusu mwenendo na mtazamo mbaya uliokuwa nao. Wengine wataona toba yako kadiri unavyoacha mazoea yanayomchukiza Mungu na unapofanya “matendo yanayoonyesha toba.”—Matendo 26:20.

  •  Ubatizo. (Mathayo 28:19) Yesu alisema kwamba wale ambao watakuwa wanafunzi wake wanapaswa kubatizwa. Mlinzi wa jela aliyetajwa hapo awali alibatizwa. (Matendo 16:33) Vivyo hivyo, baada ya mtume Petro kufundisha umati mkubwa ukweli kumhusu Yesu, “wale waliokubali neno lake kwa furaha wakabatizwa.”—Matendo 2:40, 41.

  •  Tii maagizo ya Yesu. (Waebrania 5:9) Wale ambao ‘wanashika mambo yote’ ambayo Yesu aliamuru wanaonyesha kupitia maisha yao kwamba wao ni wafuasi wake. (Mathayo 28:20) Wanakuwa “watendaji wa neno, na si wasikiaji tu.”—Yakobo 1:22.

  •  Vumilia mpaka mwisho. (Marko 13:13) Wanafunzi wa Yesu ‘wanahitaji uvumilivu’ ili         


3:Mtu Akianguka kwenye dhambi na alikuwa Ameokoka shetani humpiga mara mbili yake
Kitabu ngani kinasema hivi.

Jibu; Waebrania;6;4-6




4:Biblia Ni nini?

Jibu la Biblia

 Biblia ni mkusanyiko wa vitabu 66 vitakatifu. Iliandikwa katika kipindi cha miaka 1,600 hivi. Biblia ina ujumbe kutoka kwa Mungu—“neno la Mungu.”—1 Wathesalonike 2:13.

Tar.7/10/2024

5:TUNAJIFUNZA NINI KWA ABIGAIL
Baadhi ya wanawake wanaotajwa kwenye Biblia

Wanawake Katika Biblia—Tunaweza Kujifunza Nini Kutoka Kwao?


Jibu la Biblia

 Katika Biblia, tunasoma kuhusu wanawake wengi ambao maisha yao yanatufundisha masomo yenye thamani. (Waroma 15:4; 2 Timotheo 3:16, 17) Makala hii inazungumzia kwa ufupi tu baadhi ya wanawake wanaotajwa katika Biblia. Wengi wao ni mifano mizuri ya kuiga. Wengine ni mifano ya kuonya.—1 Wakorintho 10:11; Waebrania 6:12.



Abigaili

  Abigaili

 Abigaili alikuwa nani? Alikuwa mke wa mwanamume mkatili aliyeitwa Nabali. Hata hivyo, Abigaili alikuwa mwenye busara na mnyenyekevu, na pia alikuwa mrembo kimwili na kiroho.—1 Samweli 25:3.

 Alifanya nini? Abigaili alitenda kwa hekima na busara ili kuzuia msiba. Yeye na Nabali waliishi katika eneo ambalo Daudi, mfalme mtarajiwa wa Israeli, alikuwa akijificha. Daudi na wanaume wake walipokuwa huko, walilinda makundi ya kondoo ya Nabali yasiibiwe. Lakini Daudi alipowatuma wajumbe kumwomba Nabali chakula, Nabali aliwatukana na kukataa. Daudi alikasirika sana. Kwa hiyo, yeye na wanaume wake wakapanga kwenda kumuua Nabali na wanaume wote wa nyumba yake.—1 Samweli 25:10-12, 22.

 Abigaili alitenda upesi aliposikia kile ambacho mume wake alikuwa amefanya. Aliwapa watumishi wake chakula wampelekee Daudi na wanaume wake, naye pia akawafuata ili kumwomba Daudi awaonyeshe rehema. (1 Samweli 25:14-19, 24-31) Daudi alipoona zawadi yake, unyenyekevu wake, na aliposikia ushauri wake wenye hekima, alitambua kwamba Mungu alimtumia ili kumzuia asimuue Nabali na wanaume wake. (1 Samweli 25:32, 33) Muda mfupi baada ya hapo, Nabali alikufa, naye Abigaili akawa mke wa Daudi.—1 Samweli 25:37-41.

 Tunajifunza nini kutoka kwa Abigaili? Ingawa alikuwa mrembo na tajiri, Abigaili alikuwa na maoni yenye usawaziko kujihusu. Ili kudumisha amani, alikuwa tayari kuomba msamaha kwa jambo ambalo halikuwa kosa lake. Alishughulikia hali yenye kutisha kwa utulivu, busara, ujasiri, na alitumia nguvu zake za kufikiri.

  •  Ili kupata habari zaidi kumhusu Abigaili, ona makala yenye kichwa, “Alitenda kwa Busara.”

Debora

  

Jumapili Tar.13-10-2024

MASWALI YA BIBLIA

SWALI;

1; Ni Mwanamke Ngani Wa Kwanza Kujifungua Akafa Akijifungua Mtoto Kwenye Biblia Mtaje Jina...?


JIBU; Anaitwa Raheli Mke wa Yakobo.
Alikufa akiwa anamzaa Benjamini.

Mwanzo:35:16-19


Swali;
Dini Zote Ni Sawa Zinamwabudu Mungu wa Kweli..?

Hapana Dini zote Si Sawa.

Kutoka:20:3 Kunawanao Amini Miungu

Kutoka:32:8 Kuna Wanaoamini Mungu wa kweli.


Swali: Ni nani aliyekuambia upo uchi..?
Mungu Aliliuliza 

Mwanzo:3:11



MASWALI YA BIBLIA NA MAJIBU.


1:Inakuwaje Tunapokufa?


Jibu la Biblia

Biblia inasema: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe.” (Mhubiri 9:5; Zaburi 146:4) Kwa hiyo, tunapokufa, hatupo. Wafu hawafikiri, hawatendi, wala kuhisi chochote.


2:SWALI: Huyu Yeshuruni  ni nani kwenye biblia?. Na kwanini alinenepa na kumdharau mwamba wa wokovu wake (Kumb.32:15)?.


JIBU: Yeshuruni ni jina lingine la Taifa la Israeli lililotumika katika biblia ya kiyahudi hususani katika mashahiri,..Neno hili linaonekana mara 4 katika biblia soma (Kumbukumbu 32:15, 33:26, 33:5 na Isaya 44:2).




1:Neno Bwana lina maana gani katika Biblia?

Neno Bwana Katika Biblia linamaanisha “Mungu Mtawala”

2:Mapokeo ya Mitume ndiyo nini?

Mapokeo ya Mitume ndiyo yale yote ambayo Yesu aliwakabidhi Mitume wake, na kwa uwezo wa Roho Mtakatifu yatadumu hata mwisho wa dunia katika mafundisho, liturujia na maisha ya Kanisa.

“Nawasifu, kwa sababu mmenikumbuka katika mambo yote, nanyi mmeyashika yale mapokeo vilevile kama nilivyowatolea… Kwa maana naliwatolea ninyi hapo mwanzo yale niliyoyapokea mimi mwenyewe” (1Kor 11:2; 15:3).

“Ilinde ile amana nzuri kwa Roho Mtakatifu akaaye ndani yetu… Mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine” (2Tim 1:14; 2:2).

Tukikata huo mnyororo wa mapokeo, hata kama ni kwa kisingizio cha kushikilia Biblia, tunaachana na asili ya Kanisa.

“Basi, ndugu, simameni imara, mkayashike mapokeo mliyofundishwa, ama kwa maneno, ama kwa waraka wetu… Ndugu, twawaagiza katika jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni nafsi zenu na kila ndugu aendaye bila utaratibu, wala si kwa kufuata mapokeo mliyoyapokea kwetu” (2Thes 2:15; 3:6).

3;Maandiko Matakatifu ndiyo nini?

Maandiko Matakatifu ndiyo vitabu vyote 73 ambavyo viliandikwa na watu kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu vikakusanywa na Kanisa kwa jina la “Biblia”, yaani “Vitabu”.

Hao “wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu” (2Pet 1:21).

MASWALI NA MAJIBU YA BIBLIA 

Karibu Kipindi cha Maswali Ya Biblia Kinachotusaindia Kujifunza Biblia 
ΔΆaribu Sana Mimi Naitwa Pastor Richard Nipo Morogoro Veta Dakawa Kanisa la Holy Spirit church Tanzania 

Swali:1
   Mbinguni kukoje?Unaweza Kutupa picha Sawasawa na Andiko..?

 Jibu
Mbinguni Ni Makao ya kiroho yana utendaji mwingi sana. Yana mamia ya mamilioni ya viumbe wa roho ‘wanaolitenda neno lake Mungu’​ Soma hivi vitabu
—Zaburi 103:20, 21; Danieli 7:​10.

     "UFAFANUZI ZAIDI MAANDIKO"

 Biblia inafafanua mbinguni kuwa mahali palipo na nuru nyingi sana. (1 Timotheo 6:​15, 16) 

Nabii Ezekieli alipokea maono ya kimbingu yaliyokuwa na “mwangaza” uliong’aa sana, naye Danieli aliona maono ya mbinguni yaliyokuwa na “mto wa moto.” (Ezekieli 1:26-28; Danieli 7:9, 10)

 Mbinguni ni mahali patakatifu, au safi, na maridadi.​—Zaburi 96:6; Isaya 63:15; Ufunuo 4:​2, 3.


2:SWALI 
Je, Yesu aliishi mbinguni kabla ya kuzaliwa duniani?

JIBU LA SWALI 
 Ndiyo. Yesu alikuwa kiumbe wa roho mbinguni kabla ya kuzaliwa akiwa mwanadamu duniani. Yesu mwenyewe alisema hivi: “[Nimeshuka] kutoka mbinguni.”—Yohana 6:38; 8:23.

 Mungu alimuumba Yesu kabla ya kuumba kitu kingine chochote. Biblia inasema hivi kumhusu Yesu:

 “Yeye ndiye . . . mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.”—Wakolosai 1:15.

 Yeye ndiye “mwanzo wa uumbaji wa Mungu.”—Ufunuo 3:14.

 Yesu alitimiza unabii kumhusu yule “ambaye asili yake ni ya tangu nyakati za kale, tangu siku za zamani za kale.
”Mika 5:2; Mathayo 2:4-6.