Alhamisi, 3 Aprili 2025

SOMO MITENGO MITATU MIKUBWA

SOMO; MITENGO MATATU MIKUBWA SHETANI ANAYOTUMIA KUTESA WATEULE WA BWANA:

Hili Somo naletewa nikufundishe ujifunze kitu wakati  mwingine ili uwe  mshindi wa maisha yako jitaidi  kumjua adui yako mbinu mbalimbali anazozitumia kukushambulia wakati upo na Yesu. Itakusaindia hii.

1:MITENGO MKUBWA SHETANI HUTUMIA MANENO UJITAMKIE UDHAIFU au UTAMKIWE UDHAIFU. HESABU;30

Mfano: Hivi mawasiliano yako na mpenzi wako yanaendaje..? HUU NI MTENGO WEWE pasipo kujua unasema.

Mawasiliano saivi ananitafuta mara moja moja kikweli haya mahusiano siyaelewi.

Adui Anakunasa MAHUSIANO SIYAELEWI Hakika hutakuja kuyaelewa .

Mfano: Unatoaga zaka ?
Yaani Mwezi huu sikutoa na madeni na mama mgonjwa 

Adui anakamatia hapohapo kuongeza shida ili usitoe.

IPO HIVI KILA  MANENO UKIONGEA MABAYA  YANA Roho nyuma yake hufanya iwe hivyo ukijinasua kwenye mtengo huu ujue unielewe kweli.

2:MITENGO WA PILI NIKUZIMA MOYO WA UTOAJI WA ZAKA AU KUTOA KWA KUDANGANYA KIASI SAHIHI. 
Malaki:3:8-11 Matendo 5.

Shetani anajua wapi akikushikia huwezi kuona matokeo kama atakuacha uwe mwaminifu wa zaka atakamata kinywa chako kiwe kinajifunga nakujinenea matatizo.

Shetani anajua Mungu hupenda watu wanaomheshimu kwa zaka na Mali zao zinapeleka injili mbele ya Bwana Yesu.

NINI HUKiFANYA.

1:Kuhakikisha Anakupa mawazo unatoa zaka kwa ajili ya jambo fulani Bwana atende siyo unatoa kama sheria na upendo kwa Mungu wako.


2:Kuweka Uvivu na Upuuziaji usitowe zaka.

3:Kuleta matatizo upatapo hela ya Kutoa zaka matatizo ndiyo yanatokea kumbe linaitaji limiriki ufahamu wako na moyo wako.

4:Utaongiwa roho ya wizi wa zaka hata kama ulikuwaga mwaminifu wa zaka.
Lengo Afirisi biashara aharibu kazi yako watoto familia mke au mme nk

Uonapo haya ujuwe umeshakamatwa na shetani.

Hakikisha unainga mfano wa Matendo:10



3:MTENGO WA MWISHO KUUA KIU YA KUOMBA UTARUDI NYUMA KIMAOMBI

Wapo Watu walikuwa fire 🔥 fire katika maombi lakini saivi wamepoa kumbe katika roho wamekamatwa wanatumikishwa adui ili aviharibu vitu vyao.


TUFANYE NINI SASA SISI

Kama Mtoto Wa Mungu chochea Maombi usikubali kuimba Fungu la Kumi  Pia Usijitamkie matatizo jitabirie mazuri usijinenee uchawi kuwa umelongwa usiseme mapepo yamezuia nisiowe au kuolewa kinywani mwako toa panda mbengu njema kwa kutamka mazuri.

Kwa kufanya hivi utajinasua kwenye mitengo ya shetani mingi Lakini yaitaji umakini mno na unaweza kuniuliza inbox kama unaswali.

Naitwa Pastor Richard Wa Morogoro 
Kanisa la Holy Spirit church Tanzania 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni