Jumatatu, 29 Septemba 2025

Somo: Hedhi


           Somo: Hedhi

Dalili za HEDHI Mwanamke Kabla Hajaingia

  • Kuongezeka kwa hamu ya kula, 
  • Matiti kuuma yakiguswa, 
  • Mabadiliko ya hisia mara kwa mara, 
  • Kukasirika kirahisi,
  • Hamu ya vyakula maalumu,
  • Matatizo ya kupata usingizi, 
  • Kichefuchefu,
  • Kuishiwa nguvu,
  • Maumivu ya tumbo,
  • Maumivu ya mgongo, na 
  • Chunusi

        Visababishi VYA HEDHI KUKOMA

Kuchelewa kwa hedhi kunaweza kusababishwa na mabadiliko ya kiasili, matatizo ya homoni, magonjwa, au mitindo ya maisha. Sababu ni pamoja na:

  1. Ujauzito – Sababu ya kawaida kabisa kwa wanawake wa umri wa kuzaa.

  2. Kunyonyesha – Homoni ya prolaktini huchelewesha ovulation na hedhi.

  3. Mabadiliko ya homoni

    • Matatizo ya tezi (Upungufu au wingi wa homoni thairoidi)

    • PCOS (Sindromu ya ovari yenye vifuko maji vingi)

    • Kiwango kikubwa cha homoni prolaktini (Homoni maziwa)

  4. Matatizo ya ubongo – Uharibifu au matatizo kwenye tezi pituitari au hypothalamus.

  5. Magonjwa ya mfumo wa uzazi

    • Uvimbe au makovu kwenye kizazi (Sindromu ya Asherman)

    • Matatizo ya kuzaliwa kama kukosa uke au uterasi.

  6. Matumizi ya dawa

    • Vidonge vya kupanga uzazi (baadhi ya aina)

    • Dawa za homoni, kemotherapi, dawa za magonjwa ya akili.

  7. Mitindo ya maisha

    • Msongo wa mawazo

    • Kupungua sana au kuongezeka sana uzito

    • Mazoezi ya kupita kiasi (athlete’s amenorrhea).

  8. Kukoma kwa hedhi mapema – Komahedhi kabla ya miaka 40.


Dalili zianzoambatana na kuchelewa hedhi


Mbali na kukosa hedhi, dalili zinaweza kujumuisha:

  • Maumivu ya nyonga au tumbo

  • Matiti kujaa au kutoa maziwa bila ujauzito

  • Kubadilika kwa uzito bila sababu

  • Nywele nyingi usoni au mwilini (hirsutism)

  • Chunusi nyingi

  • Kichefuchefu, uchovu (hasa ujauzito)

  • Dalili za kukoma hedhi: moto moto mwilini, kukosa usingizi, jasho usiku

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni