Somo: Hedhi
Dalili za HEDHI Mwanamke Kabla Hajaingia
- Kuongezeka kwa hamu ya kula,
- Matiti kuuma yakiguswa,
- Mabadiliko ya hisia mara kwa mara,
- Kukasirika kirahisi,
- Hamu ya vyakula maalumu,
- Matatizo ya kupata usingizi,
- Kichefuchefu,
- Kuishiwa nguvu,
- Maumivu ya tumbo,
- Maumivu ya mgongo, na
- Chunusi.
Visababishi VYA HEDHI KUKOMA
Kuchelewa kwa hedhi kunaweza kusababishwa na mabadiliko ya kiasili, matatizo ya homoni, magonjwa, au mitindo ya maisha. Sababu ni pamoja na:
Ujauzito – Sababu ya kawaida kabisa kwa wanawake wa umri wa kuzaa.
Kunyonyesha – Homoni ya prolaktini huchelewesha ovulation na hedhi.
Mabadiliko ya homoni
Matatizo ya tezi (Upungufu au wingi wa homoni thairoidi)
PCOS (Sindromu ya ovari yenye vifuko maji vingi)
Kiwango kikubwa cha homoni prolaktini (Homoni maziwa)
Matatizo ya ubongo – Uharibifu au matatizo kwenye tezi pituitari au hypothalamus.
Magonjwa ya mfumo wa uzazi
Uvimbe au makovu kwenye kizazi (Sindromu ya Asherman)
Matatizo ya kuzaliwa kama kukosa uke au uterasi.
Matumizi ya dawa
Vidonge vya kupanga uzazi (baadhi ya aina)
Dawa za homoni, kemotherapi, dawa za magonjwa ya akili.
Mitindo ya maisha
Msongo wa mawazo
Kupungua sana au kuongezeka sana uzito
Mazoezi ya kupita kiasi (athlete’s amenorrhea).
Kukoma kwa hedhi mapema – Komahedhi kabla ya miaka 40.
Dalili zianzoambatana na kuchelewa hedhi
Mbali na kukosa hedhi, dalili zinaweza kujumuisha:
Maumivu ya nyonga au tumbo
Matiti kujaa au kutoa maziwa bila ujauzito
Kubadilika kwa uzito bila sababu
Nywele nyingi usoni au mwilini (hirsutism)
Chunusi nyingi
Kichefuchefu, uchovu (hasa ujauzito)
Dalili za kukoma hedhi: moto moto mwilini, kukosa usingizi, jasho usiku
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni