HUDUMA ZA KIROHO
Jumamosi, 14 Juni 2025
SOMO;MALAIKA MKUU RANGUEL
Jumamosi, 7 Juni 2025
MALAIKA MKUU MIKAELI
SOMO; MALAIKA MKUU MIKAELI.
KIUMBE wa roho anayeitwa Mikaeli hatajwi mara nyingi katika Biblia. Hata hivyo, kila mara anatajwa akitenda jambo fulani. Katika kitabu cha Danieli, Mikaeli anapigana na malaika waovu; katika barua ya Yuda, anabishana na Shetani; na katika Ufunuo, anapigana na Ibilisi na malaika wake waovu. Anapoutetea utawala wa Yehova na kupigana na adui za Mungu, Mikaeli anatenda kupatana na maana ya jina lake—“Ni Nani Aliye Kama Mungu?” Lakini Mikaeli ni nani?
Nyakati nyingine, watu huitwa majina mbalimbali. Kwa mfano, mzee wa ukoo Yakobo aliitwa pia Israeli, na mtume Petro aliitwa Simoni. (Mwanzo 49:1, 2; Mathayo 10:2) Vivyo hivyo, Biblia inaonyesha kwamba Mikaeli ni jina lingine la Yesu Kristo, kabla na baada ya maisha yake duniani. Hebu tuone sababu za Kimaandiko zinazotufanya tukate kauli hiyo.
Malaika Mkuu. Neno la Mungu linamwita Mikaeli “yule malaika mkuu.” (Yuda 9) Ona kwamba Mikaeli anaitwa yule malaika mkuu. Hilo linaonyesha kwamba kuna malaika mmoja tu aliye mkuu. Isitoshe katika Biblia, jina “malaika mkuu” linatumiwa katika hali ya umoja tu, wala si kwa wingi. Zaidi ya hayo, Yesu anahusianishwa na wadhifa wa malaika mkuu. Kuhusu Bwana Yesu Kristo aliyefufuliwa, andiko la 1 Wathesalonike 4:16 linasema: “Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni akiwa na mwito wenye amri, kwa sauti ya malaika mkuu.” Kwa hiyo sauti ya Yesu inafafanuliwa kuwa sauti ya malaika mkuu. Basi, andiko hilo linadokeza kwamba Yesu mwenyewe ndiye Mikaeli yule malaika mkuu.
Kiongozi wa Jeshi. Biblia inasema kwamba ‘Mikaeli na malaika zake walipigana na yule joka mkubwa na malaika zake.’ (Ufunuo 12:7) Kwa hiyo, Mikaeli ni Kiongozi wa jeshi la malaika waaminifu. Pia kitabu cha Ufunuo kinamtaja Yesu akiwa Kiongozi wa jeshi la malaika waaminifu. (Ufunuo 19:14-16) Naye mtume Paulo anamtaja kihususa “Bwana Yesu” na “malaika zake wenye nguvu.” (2 Wathesalonike 1:7) Kwa hiyo, Biblia inataja Mikaeli na “malaika zake” na Yesu na “malaika zake.” (Mathayo 13:41; 16:27; 24:31; 1 Petro 3:22) Kwa kuwa Neno la Mungu halionyeshi popote kwamba kuna majeshi mawili ya malaika waaminifu mbinguni—moja likiongozwa na Mikaeli na lingine likiongozwa na Yesu—ni wazi kwamba Mikaeli si mwingine ila ni Yesu Kristo akiwa katika wadhifa wake mbinguni. *
MASWALI NA MAJIBU YA BIBLIA
Shetani Alitoka Wapi..?
Swali: Je shetani yule audanganyaye ulimwengu alitoka wapi?
Jibu: shetani kwa asili aliumbwa na Mungu, na kabla ya kuwa shetani alikuwa akiitwa “Kerubi afunikaye”
Ezekieli 28:14 ” Wewe ulikuwa KERUBI MWENYE KUTIWA MAFUTA AFUNIKAYE; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto”.
Na MUNGU alimwumba akiwa mkamilifu (asiye na dosari) kama tu MAKERUBI wengine, lakini baadaye moyo wake uliinuka akajidanganya mwenyewe kuwa anaweza kuwa kama MUNGU (aabudiwe kama MUNGU) Na ndipo Uovu huo ukaonekana ndani yake, na hakutaka kubadilika.
Ezekieli 28:15 “Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako”
Na baadaye alipoasi ndipo akawa shetani, na maana ya shetani ni Mshitaki/Mchongezi, maana yake anawashitaki wanadamu mbele za MUNGU mchana na usiku.
Ufunuo 12:9 “Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.
10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana AMETUPWA CHINI MSHITAKI WA NDUGU ZETU, YEYE AWASHITAKIYE MBELE ZA MUNGU WETU, MCHANA NA USIKU”.
Swali la 2
SWALI LA PILI
. Tukio la Yesu kupaa kwenda mbinguni lilitukia eneo gani?. N.b weka andiko ku sapoti jibu lako
JIBU: Mlima wa mzeituni. Matendo ya Mitume 1:12 [12]Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato.
Mlima wa mizeituni..ambayo inapatika kati eneo la Bethania
Luka 24:50-51 [50]Akawaongoza *mpaka Bethania*, akainua mikono yake akawabariki. [51]Ikawa katika kuwabariki, *alijitenga nao; akachukuliwa juu mbinguni*
Swali la 3
Swali: Tunasoma Simeoni alipomwona mtoto YESU, Alikiri kuuona Wokovu wa MUNGU, sasa swali ni Wokovu gani huo alioupata?
Jibu: Tuanzie ule mstari wa 25 ili tuweze kuelewa vyema…
Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.
27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,
28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,
29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;
30 KWA KUWA MACHO YANGU YAMEUONA WOKOVU WAKO,
31 Uliouweka tayari machoni pa watu wote;
32 Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli”
Sasa hapo hajasema AMEUPATA WOKOVU..La! bali anasema “MACHO YANGU YAMEUONA WOKOVU”.. kuuona wokovu na kuupata wokovu ni vitu viwili tofauti…
Wokovu wa Mungu unapatikana kupitia mmoja tu, naye ni YESU KRISTO (Matendo 4:12),..Baada ya YESU kusulibiwa ndipo watu wakaanza kuupata wokovu, lakini kabla ya hapo waliusikia na kuuona tu,…waliousikia ni manabii wa kale na watu wote wa agano la kale, na waliouona ni watu waliokuwepo kipindi BWANA YESU anazaliwa, na walioupata ni wote waliomwamini baada ya kufufuka kw
Je Kuna Haja gani Ya Kuamini Biblia Iliyoandikwa Na Watu?
Je kuna haja gani ya kuamini biblia iliyoandikwa na watu?
Swali: Biblia imeandikwa na watu, (kama Paulo, Petro, Musa, Daudi na wengineo) je tutaamini vipi kitu kilichoandikwa na wanadamu kuwa ni kweli,? vipi kama wametoa tu kwenye akili zao, kwanini tukiamini kitabu cha namna hiyo, chenye mikono ya wanadamu?
Jibu: Kabla ya kujibu swali hili, tusome kwanza maandiko yafuatayo…
Yohana 14:11 “Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, SADIKINI KWA SABABU YA KAZI ZENYEWE”
Hapa Bwana YESU anatoa njia za sisi kumwamini yeye, kwamba kama hatutamwamini kwa yeye kutuambia kwa mdomo wake mwenyewe, basi tumwamini kupitia zile kazi anazozifanya ambazo ni ishara na miujiza.
Hiyo hakika ni hekima kuu sana!… kwamba kama sisi ni kazi sana kumwamini yeye kwa maneno ya kinywa chake, basi tuzipime zile kazi anazozifanya ikiwa ni halisi na za kweli, basi tumwamini kwahizo pasipo hata maneno yake.
Vile vile na hata kuhusiana na waandishi wa Biblia, kama hatuwaamini kuwa wameandika mambo waliyovuviwa na MUNGU, basi kupitia matokeo ya kazi hizo, (jinsi yanavyobadilisha watu wengi leo, na kuponya watu wengi) basi tuamin
Ijumaa, 16 Mei 2025
SOMO; MALAIKA MKUU URIELI.
Alhamisi, 3 Aprili 2025
SOMO MITENGO MITATU MIKUBWA
Jumamosi, 29 Machi 2025
UCHUMBA MASWALI NA MAJIBU
Jumanne, 25 Machi 2025
NDOTO ZA SHULENI
NDOTO ZA SHULENI NA MAANA ZAKE.
Karibuni Sana LEO Tuone Ndoto za Kuota Shuleni Na Maana Zake.
Ndoto huwa ni Taarifa Unayojulishwa jambo linalokuja au lilopita au lilopo
Ayubu;33:14-15
1:Ukiota Upo mazingira ya shule ya msingi na Unifom
👉👉Unajulishwa Umefungwa Usifanikiwe waitajika uombe kukemea hiyo roho.
2:Ukiota Upo shuleni unamwagilia mimea
👉👉Unajulishwa Watu Utakuwa unawafanyia kazi wezako wanafanikiwa kwa ulicho nacho wewe hutafanikiwa.
3;Ukiota Upo Palendi(Mstarini
👉👉Unajulishwa umeuganishwa na roho ya Kusimama katika hatua zako zisisonge mbele uombe uikatae hiyo roho.
4:Ukiota Upo Unacheza na Wanafunzi wezako shuleni
👉👉Unajulishwa Utateseka kwa Kuwa mpuuziaji wa vitu katika maisha yako.
5:Ukiota Upo shuleni Mwalimu anafundisha wewe huna daftari au Kalamu
👉👉 Unajulishwa Huwezi Kuweka Kumbukumbu Ya Vitu unavyoelekezwa au Kushauriwa ndiyo sababu hufanikiwi
6:Ukiota Unalia Upo maeneo ya shuleni
👉👉 Unajulishwa Unauchungu Kwakuwa Mambo hayaendi mbele kama utakavyo
7:Ukiota Upo shuleni mnafanya Mtihani wezako wanakusanya wewe Upo TU
👉👉Unajulishwa Huwezi kutatua changamoto unazopitia mpaka usaidiwe ndio utavuka kataa hiyo roho.
8: Ukiota Upo Kwenye chumba Cha Mtihani hujagawiwa Karatasi Wezako wamegawiwa
👉👉Unajulishwa Karibuni Utakutana na changamoto kabla haijakukuta Omba Kemea
9:Ukiota Upo Darasani unafundishwa somo la Hisabati
👉👉Unajulishwa Huwezi kufanikiwa Sababu huna malengo wala mikakati.
10:Ukiota Upo Darasani mnapiga Kelele Mwalimu anaingia
👉👉Unajulishwa wewe unamaneno mengi SI mtendaji wa unachokiongea ndiyo maana huendelei. Omba kemea ndoto hiyo.
11:Ukiota Upo Shule ya O,level
👉👉Unajulishwa Unamwaga wa Kufanikiwa lakini Waitaji mtu mwenye hekima akuongoze kufikia mafanikio yako
12;Ukiota Upo High School mpaka chuo
👉👉Unajulishwa Unamafanikio lakini jishughulishe na kitu Mungu atakibariki.
13: Ukiota Upo unasoma na Wanafunzi wa chuo lakini wewe hujawahi Kufika au Kusoma chuo
👉👉Unajulishwa Mafanikio yako yaitaji ukae na watu waliokuwa kiroho na kielemu utafanikiwa
14: Ukiota Upo shuleni unakula
👉👉Unajulishwa matatizo yako Yanayokutesa uliyapata ukiwa shuleni.
15;Ukiota Upo shuleni lakini maeneo ya chooni au Bafuni Ndoto ikaja hivyo
👉👉Unajulishwa Ulikanyaga Dawa ukiwa shuleni Mungu Akakukinga nazo hazijakuzuru lakini Waitaji uombee kukemea roho hizo.
16:Ukiota Upo Darasani unawafundisha wezako Mwalimu nae amekaa
👉👉Unajulishwa Utafanikiwa Kile ufanyacho Kupitia kuwasaidia watu wegine.
17:Ukiota Upo O,olevo au High school Unafundishwa na Mwalimu Wa chuo
👉👉Unajulishwa Upo unakwama kusonga mbele Kwakuwa unaitajika ukae na mtu aliyekuwa kiroho au aliyefanikiwa Kimwili ndipo utatoka kwenye pito Hilo.
18:Ukiota Upo shuleni umevaa nguo za nyumbani
👉👉Unajulishwa Unapenda Kujifunza na Kutafuta mafanikio lakini Tabia hubadiliki Unapaswa ubadilike Tabia yako Utafanikiwa
19:Ukiota wewe Ni Mwalimu Upo unafundisha shuleni kwako
👉👉Unajulishwa roho ya kutumikishwa hutaendelea kwa Kuwa unatumikishwa kila utakalokufanya. Uombe kemea
20:Ukiota wewe Mwalimu umeitwa na mkuu wako akakufokea
👉👉Unajulishwa utaitwa na mkuu wako atakuonya
NDOTO ZA SHULENI WALIZOOTA WATU ZA MASHULENI
1:Bwana Yesu asifiwe baba.Naitwa Happy Nipo Njombe Samahani naomba kujua maana ya hii ndoto nimeota usiku wa kuamkia Leo. Nimeota tulikuwa kwenye shule ya msingi niliyosoma tulikuwa Mimi na rafiki yangu, tumeenda kufundisha darasa la kwanza lakini tulipofika darasani tukamkuta mwalimu mwingine anafundisha na zilikuwa zimebaki dakika kumi na Tano tu muda wa mapumziko ufike basi tukawa tunaondoka. Lakini wakati tunaondoka tukapita nyuma ya majengo ya shule tukawa tunaona Kuna uchafu mwingi karibu kila sehemu tuliyopita kulikuwa na kinyesi Cha binadamu. Je hii ndoto Ina maana gani baba?? Inaninyima raha kabisa.
MAANA YAKE
Unajulishwa unarundishwa nyuma kiroho na hatua za maisha yako kupitia kukosa marafiki sahihi.
Tengeneza list ya watu unaoongozana nao Muombe Mungu akupe.