Ijumaa, 28 Februari 2025

SOMO; MAHUSIANO YANA LUGHA MBILI TU.

           "DARASA la UCHUMBA" 

SOMO:MAHUSIANO YANA LUGHA MBILI TU.

Karibu Mdau Wa Elimu Ya Mahusiano Mimi Mwalimu Wa Wanandoa Pastor Richard Nakukaribisha Katika Somo hili Kichwa Chetu Kinasomeka Mapenzi Yana Lugha mbili Tu. Ambazo ndiyo Zinaweza Kuharibu mahusiano na kuyafunga au Kufugulua mahusiano.
Tujifunze Pamoja.


1:LUGHA YA KWANZA NI KUSEMA "HAPANA" Hii Lugha humanisha Kukataa mtu kukukataa na mahusiano kukukataa Unapokuwa Unamahusiano yaliyogoma yatakusumbua hata kama wewe ukisema ndiyo menyewe Yakisema Hapana ni Hapana Usilazimishe.


2;LUGHA YA PILI NI KUSEMA "NDIYO"
Hii Lugha humanisha Kukubali mtu kukubali uwe naye kwenye mahusiano kwa ajili ya malengo fulani Kwa Hiyo Hii Lugha Ikikubali Ujue mahusiano utayatawala na Kuyaendesha Unavyotaka 


Chunguza upo kwenye Lugha ipi ya mahusiano kwako.

     YAKOBO;5:12
12 Zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape, iwe kwa mbingu au kwa dunia, au kwa kitu kingine chochote. “Ndiyo” yenu na iwe ndiyo, na “Hapana” yenu iwe hapana, la sivyo mtahukumiwa.


Somo hili linakupa mwanga ujue Mahusiano hayana  Lugha Moja.


Kama unaswali uliza inbox 

Alhamisi, 27 Februari 2025

SOMO: NI BORA UCHUMBA ULIOVUNJIKA KULIKO NDOA ISIYO NAAMANI MILELE.

        "DARASA LA UCHUMBA"

SOMO; NI BORA UCHUMBA ULIOVUNJIKA KULIKO NDOA ISIYO NA AMANI MILELE.
Tusome Mithali;12:1-5 Mithali;18;15 
▪︎°▪︎°▪︎°▪︎°▪︎°▪︎°▪︎°▪︎°▪︎°▪︎°▪︎°▪︎
Tunapojifunza hivi Tunapata Maarifa na ipo inakusaindia wewe unayefikiria kujiua kwa sababu ya mapenzi ni Suruhisho au Kug;ag,Ania Usipopendwa ndio upendo Acha nikuambia Mahusiano ni Darasa Pana Sana Kama ukiwa hupendi kujifunza masomo ya uchumba kutoka kwa waalimu mbalimbali ya Mahusiano yatakuliza kila Siku Sababu hayaitaji uzame rohoni yanaitaji Elimu ujifunze.

Mfano Somo la leo nafundisha ni Bora uchumba ukauvunja kama hueleweki kuliko kuingia kwenye ndoa itakayokufanya utamani kutoka Usiweze Kutoka. Kumbe Mungu alianza kusema nawewe huku mwanzo hukusikia Karibu Mwalimu Wa Wanandoa Pastor Richard Wa Morogoro. 


MAMBO MATATU KWANINI TUSEME VUNJA MAHUSIANO YASIYOELEWEKA.

1: Picha Nzima Ya Mtu Kama Mtawezana ndani ya ndoa hupimwa huku mwanzo je mnasikilizana Je Hamsumbuani Je Mnawasiliana Vizuri Kama Huku mwanzo tu mawasiliano yenu ya manati Hamsikilizani wala hakuna amani na mwezake kila mmoja Mnablock mwezi hamtafutani.

HAYA MAHUSIANO VUNJA SABABU YATAKAPOENDELEA YAKAINGIA KWENYE NDOA YATAKUTESA.


2:Kama Mahusiano Yako Hayaeleweki Maana Yake Kati Yenu Hayupo Tayari Kuingia Kwenye Maisha Ya ndoa Na ukilazimisha Mahusiano Hayo Ujue Ndoa ndani haitakuwa na Amani.

3:Ni Bora Ukavunja Uchumba Kama Hueleweki Kuliko Kuja Kuishi na ndoa itakayokutesa milele eti kisa ulikuwa umri umeenda ukaona uwafurahishe wazazi uolewe.

4: Tambua Usiingie Kwenye Uchumba na Mtu uliyetafutiwa au Kuuganishwa na mtu wewe hukumpenda ukaamua umpende kwa Sababu ya Heshima ya Huyo Mtu.

5: Jinsi Utakavyokuwa Strong Kwenye Uchumba ndivyo utakavyokuwa Imara Kwenye Ndoa.

              TAHADHALI;
Uchumba Siyo Ndoa na Hakuna Kifungo Kitakachokutesa Ukivunja Kuliko Agano la ndoa uje uhagaike kulivunja Kiroho Husumbua Sana.


Shirikisha ujumbe huu ukiwa unaswali Uliza inbox

Jumanne, 25 Februari 2025

SOMO: SHUKURU KWA KIDOGO

SOMO: SHUKURU KWA KIDOGO.

Naitwa Pastor Richard Wa Morogoro  Kanisa la Holy Spirit church Tanzania. 
Karibu Tujifunze kitu

Jifunze Kuwa Unamshukuru Mungu Vitu vidogo Mungu Anavyokutendea Ipo nguvu mwana wa Mungu Kuthamini hatua mbalimbali za ukuaji wa kiroho kwako na utendaji wa ukuu wa Mungu kwako.

Zaburi;50:14-15
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu,
timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
15 na uniite siku ya taabu;
nami nitakuokoa, nawe utanitukuza

HATUWEZI TUKAWA TUNASUBIRIA MPAKA MAKUBWA TUTENDEWE NDIYO TUSHUKRU.

Tupo watu hata kuomba tulikuwa hatujui Ametufunza kuomba lakini bado hatuoni kama ametenda.

Tupo Watu Tulikuwa hatuna hata wachumba Tumepata Wachumba lakini bado hatuoni hilo kama Ametenda.

Tupo Tuliokuwa Kazini Tumekosa Kibali Sasa Tunakibali bado hatuoni hilo kama Ametenda.

Tupo watu Tulikuwa Hatupendi Neno la Mungu hata kujifunza Sasa hivi mioyo yetu inapenda kujifunza lakini bado hatuoni kama Ametenda.

Tupo watu familia Zetu Zilikuwa Zinateseka Lakini Sasa hivi familia zetu zimefunguliwa lakini bado tunamanug,uniko hatuoni hilo.

HVI VIDOGO TUSIPOSEMA ANSATE BWANA TUNAZUIA MIUJIZA YETU MIGINE.

Mwanangu Hebu Badili Mtazamo Wako Uwe Unashukuru Mungu.
.Soma hili Neno.

1TIMOTHEO:4:4-5
4 Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani, 

5 kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba

KILA MABADILIKO YAKO YANAITAJI MUNGU AFANYE UNAPOONA RUDI MAGOTINI NA SADAKA YA KUSHUKURU SEMA BWANA

 Nashukuru Kwa hatua hii Uliyoitenda Kwangu nilikuwa siombi saivi naomba nilikuwa sipati kazi nimepata kazi mtu mwigine akipata kazi privet Bado Anamlalamikia Mungu.

Acha Kuwa Unanug.unika na Kulia Lia Wewe ni mtoto wa Mungu ifikie hatua utambue wewe ni nani katika ulimwengu huu wa damu na nyama. 
Mungu Anasema Mwanangu nijue Vizuri Baba Yako.

Moja ya jambo mhimu ni wewe kujua kushukuru katika kila hatua.

WAKOLOSAI:4:2-3

2 Dumuni sana katika maombi, mkikesha katika hayo pamoja na kushukuru. 

3 Pia tuombeeni na sisi ili Mungu atufungulie mlango wa kunena, ili tupate kuitangaza siri ya Kristo, ambayo kwa ajili yake pia mimi nimefungwa.

TUSIPOTENGENEZA ENEO HILI TUTAKWAMISHA VITU VINGI.

Pia acha kulalamika na kunug,unika Tambua Kazi ya Mungu Kwako anayokufanyia ni kubwa Sana Siyo Jambo la wewe mwanae unayemjua vyema kukata tamaa au kumuacha hili Lichukue litakusaindia 

Mapito na changamoto zisiwe Sababu Za Kufuta mazuri yote uliyofanyiwa na Mungu

Huu mstari hebu urudie rudie utafakari kwa kina maana nasikia sauti inaniambia waambie watu wangu ulionipa uwaongoze kwa Neno la Langu Wawe na Moyo Wa Kunishukuru na Kutambua Najishughulisha na maisha yao kuliko nguvu zao na akili zao na Elimu zao Japo hawaoni wananilalamikia Sitendi kwao.

AYUBU;22;21-22

.21 “Mjue sana Mungu ili uwe na amani,
ndipo mema yatakapokujia.
22 Uyapokee mafundisho toka kinywani mwake,
na maneno yake uyaweke moyoni mwako

Jumatano, 19 Februari 2025

MAOMBI YA USIKU WA MANANE 2025

MAOMBI YA USIKU WA MANANE LEO.2025
SAA;6;00Usiku mpaka

Saa;10:00Alfajiri

Ukiamka Huu Muda ingia Vitani Ombea kila Jambo unaloona haliendi Waunge na rafiki zako Kwenye Group wanaopenda masomo na Maombi unawapa utaratibu kabla hujawaunga

Karibu Sana Tambua Usiku huwa ndiyo muda mzuri Wa Mungu Kuwashughulikia Adui Zako na Matatizo yako kuyashughulikia.

HAKIKISHA UMEOMBA TOBA KABLA HATUJAANZA KUPINGA NA KUSHAMBULIA

MSTARI WA KUSIMAMIA Kutoka;11;4

4 Kwa hiyo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Panapo usiku wa manane Mimi nitapita katika nchi yote ya Misri.

Rudia kusoma chukua point hii Mungu Apite kwako

TUTAOMBEA MAMBO  MATATU

1;Roho Ya Uzuizi Kwenye Wokovu Wako.

Ulishawahi Kujiuliza Kwanini mliokoka wengi wezako walishaacha Wokovu wakawa watumwa wa dhambi wewe unaendelea vizuri nakujitakasa mara kwa mara.

Ipo hivi Unapookoka Shetani huandaa roho chafu mbalimbali za kuhakikisha Huendelei Mbele Na hutumwa vitu mbalimbali vya kukatisha tamaa na kupelekea uache wokovu.

OMBEA WOKOVU WAKO UWE IMARA USIJE UKAWA MSINDIKAJI.

2;Roho ya Kuzuia Kutenda Matendo Mema.

Ipo roho hupandikizwa ndani yako unapokuwa umeamua kutembea na Mungu Ambayo itakufanya tu njia zako zisiwe Sahihi hata kama umeokakaje Matendo yako yatakuwa na udhaifu Tu.

Ombea Matendo yako Yawe na Kibali Kwa Mungu.

3:Roho za Mafatilizi ya Hatua Unazokuwa Unachukua

Mtoto wa Mungu Zipo roho Hufatilia Kila steji unayotaka uifanye omba shugulikia.

Ndio Maana Unaweza ukaanzisha Jambo unaamua kuliacha au Uchumi unapigwa kiasi kwamba hata hela ya Kula Unaanza Kukopa ule.

Jitaidi Kuwa Siriazi Na Upende Kuongezeka Kiimani Sikiliza Muongozo wa Maneno Roho Mtakatifu anayokupa wakati ukiomba usiku.

FAIDA ZA KUOMBA USIKU WA MANANE
Matendo;16;25-26

1;Maombi ya Usiku wa Manane Yana nguvu yakukufungua Matatizo yako Mengi.

2:Maombi Ya Usiku Ni Tulivu unakuwa husumbuliwi upo uweponi.

3:Mungu hupita kuwatandika adui zako vibaya mno.

4;Unapata mume au mke kupitia kuomba usiku wa manane.
Samsoni na Delila walipatana Usiku wa manane.

5;Unajimarisha kiroho na Kimwili katika Vita za Kiroho.

6:Unakuwa na nguvu ya kuomba Sana..

Taja nawewe unazozijua

Omba nasi Usiku wa Manane kila Siku.
.
HOLY SPIRIT CHURCH TANZANIA ILIPO NASISI TUPO HAPO.

Moto Wa Yesu Uwake Zaidi ya Jana.

2025 Tunatembea Kibabe
Mathayo;11;12

Shirikisha na wengine muombe Pamoja na rafiki zako.

.Mawasiliano na Bishop Richard Mwenyewe 0759861768 au Tigo 0710889892

Jumatatu, 17 Februari 2025

OMBA UKIWA UNAHITAJI KUPAKATA MTOTO

OMBA UKIWA UNAHITAJi KUPAKATA WATOTO WATATU MAPACHA KAMA HANNA

Tumia Baraka Ya Hanna na Mfano Wa Maombi Yake.

          1SAMWELI:2:21
21 Bwana akawa mwenye neema kwa Hana, naye akapata mimba akazaa wana watatu na binti wawili. Wakati huo, kijana Samweli akaendelea kukua mbele za Bwana.

TAMKA MANENO HAYA UKIWA UMESHIKA TUMBO.
Omba haya maombi kisha tafuteni mtoto na mumeo utapokea muujiza huu.

Sema hivi: Bwana Kuwa Mwenye Neema Kwangu Nibariki Tumbo langu Kama Hana ulivyomkumbuka ukampa Mapacha watatu mara 2 Nami Nipe Watoto mapacha watatu maana moyo wangu nimekuwa mwaminifu katika maombi kukumbusha nimekuwa mwaminifu wa zaka katika madhabahu yangu kwa Baba yangu wa kiroho uliyenipa Pastor Richard kama Hanna alivyokuwa mwaminifu kwa Baba Yake Wa Kiroho Elly  Nami Sitaacha Kukusifu na kukutolea shukurani kama Hanna.Ninaomba Nikiamini  Kwa nguvu ya Jina la Yesu.Amen 
Rudia ×4 Tamka kwa kuikaza sauti yako na kwa mamlaka.


JIANDAE KULEA MAPACHA

Nifate inbox ukiwa hujanielewa Mwanangu