Jumatatu, 27 Novemba 2023

Somo;KUIONDOA NADHIRI

SOMO: JINSI YA KUIONDOA NADHIRI KWA BWANA 

Inawezeka Ulishawahi Kuweka Nadhiri halafu ukajisahulisha hukuiondoa na Sasa Mambo yako unaona yanafunga Kwa Sababu ya Nadhiri Karibu Tuondoe Nadhiri Zetu.


Muhubiri:5:4 Ayubu;22;27 Hesabu.30 1samweli;1:11

Nadhiri ni Kiapo cha Nafsi kati yako na Mungu Kumweleza Akifanya jambo fulani nawewe utafanya.

UTOFAUTI KATI YA AHADI NA NADHIRI.

AHADI Ni Makubaliano ya kufanya Jambo fulani mkimshirikisha Mungu katika makubaliano hayo munaweza kuwa wawili au kundi mmoja wenu akaahidi atafanya jambo.

Ambayo huwa inaenda kuwa kifungo kwake kama hatafanya Soma Sura yote Hesabu:30


NADHIRI Ni Kiapo unachomuapia Mungu Kati ya Nafsi yako na Mungu unaweza kutamka haya maneno Peke Yako Kuwa Mungu Ukinipa mume mwaka huu nikaolewa nitakufanyia hili au ukiniokoa nikaacha hiki nitakutumikia Hicho ni Kiapo ukiacha Kufanya utamfanya Mungu akuadhibu Sana.


JINSI YA KUIONDOA NADHIRI. 

Kumbukumbu la Torati 23:21

[21]Utakapoweka nadhiri kwa BWANA, Mungu wako, usiwe mlegevu katika kuiondoa; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, hataacha kuitaka kwako; nayo hivi itakuwa dhambi kwako. 

1;Utafanya Kama Ambavyo ulimuwekea nadhiri Mungu. ULICHOKISEMA NDIYO UTAKACHOKITENGUA KWA KUKIFANYA.

Soma 1Samweli;1:11


2.Usichelewe Ukiona Dalili za ulimwambia Ameanza Kulifanya nawewe Tafuta hiyo Nadhiri uiondoe.

Ayubu:22:27 Muhubiri;5:4


3.Utaitowa Kwa Baba Yako wa Kiroho Ambaye mtumishi Mungu Amekupa au Uwasiliane na Pastor Richard akupe maelekezo kama huna Baba wa Kiroho.

Matendo;18;18 Zaburi:61;5

MAMBO YA KUFANYIA KAZI KABLA HUJAIONDOA


1:TAFADHALI KAMA HUJUI KUIONDOA NADHIRI AU HUNIELEWA USIFANYE NIPIGIE SIMU NIKUELEKEZE NA USICHANGANYE AHADI  NA NADHIRI. 

2:KILA NADHIRI ULIYOIWEKA INAMAELEKEZO YAKE NAMNA YA KUOMBA UNAPOIONDOA UTANIPIGIA UNIELEZE NADHIRI YAKO KISHA NITAKUPA MUONGOZO 

3:NADHIRI USIPOIONDOA HUWA KIFUNGO KIBAYA SANA NA HUKUPELEKA KUITWA MWENYE DHAMBI.


4:TAFADHALI NI BORA USIWEKE NADHIRI KULIKO UWEKE UWE MLENGEVU KUIONDOA.


5:NADHIRI HUENDELEA KUDAI HATA KAMA UKIPOTEZEA MUNGU HAPOTEZEI.

6;NITUMIE WHATSAPP UJUMBE KABLA HUJANIPIGIA KWA 0759861768 


MAOMBI YA KUOMBA UNAPOIFUTA NADHIRI AMBAYO HAIJATIMIA.

Baba Yangu Uliye mbiguni Ninafuta Kila maneno niliyoyatamka Kupitia kuweka Nadhiri yangu japo hukujibu na hukutenda naelewa Sababu hukutaka iwe kwa majira niliyoyataka mimi Bwana Naabatanisha Sadaka Yangu Hii Kupitia Kufuta hii Nadhiri Naomba ipokee Katika Madhabahu hii ya Moto wa Yesu Katika Jina la Yesu.Amen 


Kisha itume Sadaka yako kwa Tigo Pesa +255710889892  Halo Pesa 0628355985
Jina Richard Julius Kushoka 


KAMA NA MUNGU AMEJIBU NADHIRI YAKO

Baba yangu Nakushukuru Kujibu Maombi yangu Na Kuitimiza Nadhiri yangu ninaomba Bwana niondoe na ninafanya kama nilivyokuwa Nimeapa ukinifanyia au ukinipa ....Nitafanya hivi(Taja) Naitoa na kuitengua Nadhiri yangu kwenye madhabahu hii ya Holy Spirit church  Naomba ipokee ikatende Kwenye madhabahu yako ya Moto wa Yesu Ameni

Utanipigia kabla hujatuma hii sadaka.



HITIMISHO 

Mimi ninaona vyema Sana nadhiri yako ukaiondoa kuliko unavyojifanya kama hujawahi kuweka nadhiri  na kama hujawahi kuweka sikushauri uweke nadhiri kabisa.


Wito
Wito wangu wote Tujifungue na nadhiri zetu zote tuanze upya na Bwana 
Naitwa Pastor Richard Nipo Morogoro Veta Dakawa 
Kutoka Kanisa la Holy Spirit church Tanzania 

Wapo watu wanateswa na laana ya nadhiri zao hawajawahi kuziondoa. NIULIZE SWALI LA NADHIRI KUONDOA 


Share somo hili

Jumamosi, 18 Novemba 2023

SOMO;KANUNI NANE ZA KUFANIKIWA.

Kanuni NANE (8) za kufanikiwa katika maisha.

Utangulizi
Maisha na mafanikio ni vitu viwili tofauti lakini vinavyoenda sambamba siku zote. Kila mwanadamu anatamani afikie malengo fulani ambayo anajiwekea katika maisha yake. Malengo hayo huwa hayafanani kwa watu wote hivyo mafanikio ni tofauti kwa watu tofauti. Kwamfano mwanafunzi anaweza akapanga kufikia maadhimio Fulani katika masomo yake na mwingine akapanga kupata zaidi kulingana na anavyoona uwezo wake. Anapofikia malengo aliyojiwekea, hii inamaanisha kwamba amefanikiwa. Lakini unaweza kujikuta mara nyingi umepanga mipango mingi lakini haufanikishi hata mpango mmoja kati ya mipango hiyo uliyoipanga. Swali ni je, ulifuatisha kanuni za kufanikiwa? Ulijiandaa kufikia malengo uliyojipangia? Kanuni zifuatatazo zinaweza kukusaidia kufika sehemu katika mipango yako kama kweli utatilia maanani.

                             

1.      Fanya kazi kwa bidii.
Watu wengi tumekuwa tukifanya kazi kama kutimiza ratiba tu za kila siku na wengine tunafanya kazi tu kwakuwa mwisho wa mwezi tutapata mshahara. Na wengine tunafanya kazi ilikusudi tusionekane tunashinda tu nyumbani na kuanza kuitwa yale majina ya “goli kipa” na mengine mengi. Lakini katika kufanya kazi hizo tunakuwa hatuweki juhudi na kuzifanya kwa bidii matokeo yake tunakosa ufanisi na umakini katika kazi hizo tunazozifanya.
Wengine wanashindwa kuweka bidii katika kufanya kazi walizonazo kwasababu tu walilazimishwa labda na wazazi wao kuchukua fani fulani walipokuwa wanajiunga na elimu ya juu. Hivyo kufanya kazi ambazo hawazipendi, hivyo wanajikuta wanafanya tu ilimradi siku iende lakini hawazipendi. Je, unawezekana kuweka bidii katika kitu ambacho haupendi? Jibu sahihi hapa itakuwa ni hapana. Kufanya kazi kwa bidii kunahitaji utayari wa kufanya kitu kutoka moyoni. Mtu akishindwa kufanya kazi kwa bidii itakuwa ni vigumu sana kufikia malengo aliyojipangia katika maisha na mtu kama huyo asahau kabisa maendeleo katika maisha yake.

2.      Ishi kulingana na kipato chako.
Watu wengi wanapenda kuishi maisha ambayo ni ya juu kuliko kipato chao walichonacho au wanachoingiza kila mwezi. Hivyo kila mwisho wa mwezi unajikuta unapokea mshahara au hesabu zako zote za mwezi zinaishia kulipa madeni hakuna faida. Tatizo ni nini hasa? Ulijaribu kuishi maisha ambayo si maisha yako. Kama ungekuwa unaishi maisha ambayo hakika ni ya kwako basi ungetulia na kukipangilia kile kipato chako unachopata kwa mwezi na kutosha. Kwamfano unagawa mshahara wako au kipato chako kwa mwezi na matumizi yako na kuhakikisha kwamba kipato kinatosha na unapata akiba. Unaweza ukaainisha matumizi yako kwa mwezi, ukagawanya kwa kutumia asilimia na ukapata mgawanyo wa hela yako au kipato chako.

3.      Usiige namna ya kuishi.
Kila mtu ana namna yake ya kuishi kwahiyo hakuna mtu hata mmoja atakuwa sawa na mwenzake hata ukijilazimisha kufanana na mtu mwingine haiwezekani kwani hata mapacha wa kufanana hawawezi kuwa na maisha sawa au mafanikio sawa katika maisha. Katika maisha ya uanafunzi kila mtu anatamani angekuwa wa kwanza lakini kinachotokea ni kwamba hata kama wanafunzi wote watapata alama sawa darasani wa kwanza hadi wa mwisho ataonekana tu. Malengo tuliyonayo yanatofautiana kutoka mtu mmoja na mwingine kwahiyo unapojaribu tu kuishi maisha ya mtu mwingine unajikuta unapoteza mwelekeo na malengo yako hivo kushindwa kufikia mafanikio katika kile ulichopania kufikia kwa kipindi fulani.
Ukiishi maisha yako utaweza kuwa na msimamo wa kile unachopanga kufanikisha katika masiha. Hautakuwa tayari kubadilishwa mtazamo wako na mtu yeyote kwasababu utakuwa unajua kitu unachofanya, utakuwa na mtazamo chanya kuelekea mafanikio yako.

4.      Fanya kitu ambacho unaweza si kama vile watu watakavyo.
Mara nyingi katika maisha tumejikuta tumefanya vitu ili kuwafurahisha watu wengine na si kwasababu tunauwezo wa kufanya vitu hivyo. Wewe mwenyewe ndiye unajua mapungufu au udhaifu wako na uwezo wako wa kufanya jambo fulani. Kwahiyo kusikiliza sauti za wengine mara nyingi hupelekea kufanya kitu ambacho wewe hauwezi. Kwa mfano unaweza kuwa ni daktari mzuri lakini mwongeaji; kwasababu ya hali yako ya uchangamfu na kuongea na watu vizuri, kuwa na lugha ya ushawishi basi watu wanakushauri wewe uwe mwanasiasa. Kumbuka si kila mtu mwongeaji basi anawezakuwa mwanasiasa na siyo kila mtu mkimya anaweza kuwa daktari.
Kusikiliza ushauri wa watu wengine ni jambo zuri na la msingi sana, lakini kufanya vile wanavyotaka wengine ni jambo la hatari sana katika maisha. Kumbuka wewe mwenyewe ndiye unayejijua ulivyo na hakuna mtu mwingine anayekujua wewe. Sisi watu wengine tunachokiona ni matokeo ya maamzi yako wewe. Hivyo kukujua wewe ni pale tu unapofanya maamzi yako.
Mfano mzuri ni kwenye mpira wa miguu, kama wewe ni mfungaji hauwezi kulazimishwa na watu ukakae golini. Kufungwa utafungwa tu kwasababu unatenda kazi katika nafasi ambayo siyo ya kwako bali unatakakutimiza tu wanayotaka watu unaowasikiliza. Wewe mwenyewe unajua kuwa kudaka hauwezi kabisa lakini unakaa kwasababu tu umewasikiliza watu wanasemaje. Kama unafanya mambo yako ili kiiridhisha jamii au watu wanaokuzunguka, sahau mafanikio.

5.      Epuka starehe.
Starehe ni moja kati ya changamoto kubwa sana katika kufanya watu wasiendelee, hii hupelekea watu kutumia pesa zao vibaya. Si pesa tu bali hata kupoteza muda mwingi ambao kama ungetumika kwa kufanya mambo ya msingi ungevuka hatua moja katika maisha yako. Starehe siku zote inahitaji pesa na muda, ukiwa kwenye starehe huko unakutana na ushindani mkubwa wa watu wanaotumia pesa, wewe pamoja na kutokuwa na pesa za kutosha za mengineyo, utajikuta unatumia pesa hadi za akiba na mwisho wa siku unaambulia madeni yasiyokoma.
Mfano mzuri ni kuingia kwa simu za kisasa (Androids, Smart Phones, Tablets, nk) kumepelekea vijana wengi (kwa ulimbukeni) kuzinunua na kujiunga kila mtandao wa kijamii. Siyo vibaya lakini matumizi yake yamekuwa kinyume na kumfanya kijana kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi huku akichati mambo yasiyofaa na kutumia pesa nyingi sana katika kununua kifurushi vya mtandao “Internet”

6.      Uwe na nidhamu ya pesa.
Kila mtu anahangaika kuitafuta pesa kila iitwapo leo. Wakati pesa hiyohiyo ikiwa ngumu kwa watu fulani fulani kwa wengine siyo shida kubwa kwani wanaweza kuipata kiurahisi. Wakati wengine wakidharauliwa kwa kutokuwa na pesa wengine wanaheshimiwa na kuabudiwa kwakuwa nazo hizo pesa. Lakini kitu cha muhimu sana katika pesa ni “NIDHAMU YA PESA”
Pesa siyo mbaya lakini maamzi anayoyatoa mtumiaji wake huwa ni mabaya sana. Hivyo pesa hizohizo zimekuwa laana kwa baadhi ya watu na kwa wengine zimekuwa Baraka. Kinachofanya kwa wengine iwe Baraka na wengine iwe laana ni matumizi yake. Kukosa nidhamu ya pesa na kuitumia ovyoovyo hupelekea mtu kujenga uadui na watu wengine na kujitenga kabisa mbali na Mungu. Katika kufikia mafanikio lazima tuwe na nidhamu katika kuzitumia pesa.

7.      Fikiri juu ya maisha ya baadaye.
Wahenga walisema “fikiri kabla ya kutenda” na katika maisha pia mtu anashauriwa kuwa na picha kichwa ya aina ya maisha ambayo anataka kuja kuishi. Lazima kila jambo unalofikiria na kulifanya liwe na malengo fulani katika maisha yako. Kabla ya kufanya maamzi ya suala lolote lile unatakiwa uwe na mipango ya nini unataka kufanya na unataka kuishi maisha ya aina gani hapo baadae. Je, una tamani ukiwa mzee wajukuu wako wajifunze nini kutoka kwako? Unataka jamii inayokuzunguka isemeje kuhusu wewe? Je, unata uje kudharaurika au kuheshimika?
Matokeo ya kufikiria kwako ndiyo yatakayokupa picha halisi ya maisha ambayo utakuja kuishi. Kufikiria vibaya siku zote humpelekea mtu kuishi maisha mabaya na matokeo ya kufikiria vizuri siku zote hupelekea maisha mazuri.

8.      Angalia watu unaoandamana nao.
Siku zote wale unaoandamana nao utakuwa kama wao. Hauwezi hata siku moja ukajadili mambo ya msingi wa watu wapuuzi. Siku zote uandamane na watu waliofanikiwa katika eneo ambalo unafanyia kazi. Inawezekana ni ofisini au biashara, kilimo na shughuli nyingine. Watu waliofanikiwa (siyo wote, bali wale wenye mtazamo chanya kuelekea wengine) si kila mtu aliyefanikiwa basi atataka na wewe ufanikiwe kwa jamii nyingi za kiafrika kwani wengi wanatamani wafanikiwe peke yao. Usijifanyie urafiki na mtu mpaka pale utakapokuwa umezisoma njia zake.
Siku zote ukiandamana na watu walioshindwa watakuwa wanakukatisha tamaa na watakufanya usiendelee mbele. Marafiki unaojifanyia siku zote wanatakiwa wawe na mawazo na mtazamo chanya. Lazima wasiwe watu wa kukata tamaa bali wawe na msaada kwako hata kimawazo